Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko (wa pili kulia) akionyesha moja ya maghara yatayovunjwa ili kupisha maboresho ya kuifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa ya kisasa na yenye uwezo wa kupokea meli kubwa zaidi aina ya ‘Panamax’. Wanaomsikiliza pichani ni Wakurugenzi wa Bodi ya TPA wakiongozwa na Mwenyekiti wao Prof. Ignatus Rubaratuka (katikati) mara baada ya kufanya ziara bandarini hapo kukagua miradi ya maendeleo na utekelezaji wa huduma ya shehena bandarini hapo.
Naibu Mkurugenzi Mkuu (Miundombinu) wa TPA, Mhandisi Karim Mattaka akitoa maelezo kwa Wakurugenzi wa Bodi wa TPA mara baada ya kufanya ziara bandarini hapo kukagua miradi ya maendeleo na utekelezaji wa huduma ya shehena katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko (kulia) akionyesha moja ya maeneo yatakayofanyiwa ukarabati wa kuifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa ya kisasa na yenye uwezo mkubwa zaidi wa kuhudumia meli kubwa aina ya ‘Panamax’ kwa Bodi ya Wakurugenzi wa TPA, mara baada ya Bodi hiyo kufanya ziara bandarini hapo kukagua miradi ya maendeleo na utekelezaji wa huduma ya shehena bandarini. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TPA, Prof. Ignatus Rubaratuka na Naibu Mkurugenzi Mkuu (Miundombinu), Mhandisi Karim Mattaka.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TPA, Prof. Ignatus Rubaratuka (kulia) akikagua miradi ya maendeleo na utekelezaji wa huduma ya shehena ya Bandari ya Dar es Salaam pamoja na Wakurugenzi wake wa Bodi na Menejimenti ya TPA.
Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko (kulia) akionyesha Wakurugenzi wa Bodi ya TPA eneo litakalojengwa mizani ya kisasa kwa ajili ya kupima uzito wa mizigo inayotoka na kuingia bandarini mara baada ya Bodi ya Wakurugenzi kufanya ziara bandarini hapo kukagua miradi ya maendeleo na utekelezaji wa huduma ya shehena bandarini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...