Na Mwandishi Wetu – Dodoma

Agizo alililotolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu la kuanzishwa kwa madawati ya kijinsia katika shule za Msingi na Sekondari nchini alilotoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa kike Novemba 2017 Mkoani Mara limeanza utekelezaji wake.

Utekelezwaji wa agizo hilo umeanza kwa kuanzishwa kwa Programu ya kuwajengea uwezo walimu na wanafunzi wa shule za Sekondari katika kukabiliana na  ukatili shuleni ambapo ndipo vitendo vingi vya ukatili ufanyika.

Programu hiyo iliyoanzishwa na Shirika la World Education na kuishirikisha Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yenye lengo la kuwajenga uwezo watendaji wanatekeleza afua za ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto kuwa na mbinu za kuzuia, kuchukua hatua na kushughulikia wahanga wa ukatili shuleni.

Akifungua kikao baina ya Wizara na Shirika la World Education kujadili Programu hiyo jijini Dodoma, Kaimu Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Marcel Katemba amesema kuwa Programu hiyo itasaidia kwa asilimia kubwa  kuweka mazingira salama na rafiki kwa watoto kusoma bila kusumbuliwa na  aina yoyote ya ukatili shuleni.

Ameongeza kuwa kupitia vitini vilivyopo katika Programu hiyo vitasaidia kuongeza weledi wa walimu kwa kubadili mitazamo na tabia zao na kuwa zenye nia ya kupinga vita ukatili na kuwa tayari kushughulikia vitendo vya ukatili punde vinapotokea.
 Kaimu Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Marcel Katemba akifungua kikao baina ya Wizara na Shirika la World Education kujadili Programu ya kuwajengea uwezo waalimu na wanafunzi wa shule za Sekondari kupambana na ukatili shuleni kilichofanyika Jijini Dodoma.
 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mtoto, Margareth Mussai akielezea jinsi ukatili kwa watoto unavyoleta  athari kubwa kwa watoto wakiwa wadogo na wanapokuwa watu wazima katika kikao baina ya Wizara na Shirika la World Education kujadili Programu ya kuwajengea uwezo waalimu na wanafunzi wa shule za Sekondari kupambana na ukatili shuleni kilichofanyika Jijini Dodoma.
 Mtaalamu wa masuala ya Elimu kutoka Shirika la World Education, Grace Muro akitoa taarifa ya hali ya ukatili kwa watoto ya mwaka 2011 ikionesha kuwa msichana 1 kati ya 3 na mvulana 1 kati ya 7 walifanyiwa ukatili wa kingono kabla hawajafikisha miaka 18 katika kikao baina ya Wizara na Shirika la World Education kujadili Programu ya kuwajengea uwezo waalimu na wanafunzi wa shule za Sekondari kupambana na ukatili shuleni kilichofanyika Jijini Dodoma.
 Mwakilishi Mkazi wa Shirika la World Education Tanzania, Lilian Badu akielezea dhumuni la Shirika lake kutekeleza Programu ya kuwajengea uwezo waalimu na wanafunzi wa shule za Sekondari kupambana na ukatili shuleni katika kikao kati ya Serikali na Shirika hilo kujadili Programu hiyo kilichofanyika Jijini Dodoma.
 Mtaalamu wa Masuala ya Kijinsia kutoka Shirika la Plan International Tanzania Dkt. Katanta Simwanzi akielezea masuala mbalimbali ya ukatili wa kijinsia na jinsi uanvyoleta madhara kwa jamii katika kikao baina ya Wizara na Shirika la World Education kujadili Programu ya kuwajengea uwezo waalimu na wanafunzi wa shule za Sekondari kupambana na ukatili shuleni kilichofanyika Jijini Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Wadau kutoka Shirika la World Education wakijadilaina kuhusu utekelzaji wa Programu ya kuwajengea uwezo waalimu na wanafunzi wa shule za Sekondari kupambana na ukatili shuleni katika kikao kilichofanyika Jijini Dodoma. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...