Baadhi ya wabunge wakimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) na Naibu wake Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), baada ya kupitishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2018/19 Bungeni, Dodoma ambayo imeweka kipaumbele katika maendeleo ya  uchumi wa viwanda.  
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (kushoto), akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Kilimo  Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (katikati), na Mhe. Janeth Masaburi baada ya kupitishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2018/19 Bungeni Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako, wakiwa na furaha katika viwanja vya Bunge baada ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2018/19 kupita Bungeni Dodoma.

 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akipeana mkono wa pongeze na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Doto James baada ya Bunge kupitisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2018/19, Jijini Dodoma.
Kamishna wa Bajeti, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Mary Maganga, (kulia) akibadilishana mawazo na Kamishna Msaidizi wa Bajeti wa Wizara hiyo Bw. Pius Mponzi (katikati), nje ya ukumbi wa Bunge, baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa tatu kulia), na Naibu wake Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (wa tatu kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (wa pili kushoto), pamoja na Maafisa waandamizi wa Wizara hiyo wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Bunge kupitishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2018/19, Jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...