Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro leo Ijumaa Juni 1,2018 amekabidhi msaada wa nguo za shule na kadi za bima ya afya kwa wanafunzi 200 wanaoishi katika mazingira magumu katika kata za Chamaguha,Ibadakuli,Kizumbi, Mwawaza na Mwamalili zilizopo katika manispaa ya Shinyanga.
Msaada huo umetolewa na Shirika la lisilo la kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la mjini Shinyanga linalotoa huduma za kijamii kwa vijana ,watoto na wanawake na makundi yasiyojiweza.
Akizungumza wakati wa Tamasha lililokwenda sanjari na ugawaji wa sare za shule na kadi za bima ya afya,Matiro alisema bado wilaya yake inakabiliwa na changamoto ya mimba na ndoa za utotoni huku miongoni mwa sababu zinachochangia ikiwa ni ugumu wa maisha.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro akikabidhi msaada wa nguo za shule na kadi za bima ya afya kwa wawakilishi wa wanafunzi 200 wanaoishi katika mazingira magumu katika kata za Chamaguha, Ibadakuli, Kizumbi, Mwawaza na Mwamalili zilizopo katika manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro akiendelea kuzungumza wakati wa tamasha la TVMC.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro akishikana mkono na mmoja wa wanafunzi wakati wa zoezi la kugawa kadi za bima ya afya watakazozitumia kwa ajili ya matibabu
Mwanafunzi akishikana mkono na Katibu wa siasa na uenezi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini,Rajabu Bwanga baada ya kupata kadi yake ya bima ya afya.
.
Mkurugenzi wa Shirika la TVMC Mussa Jonas Ngangala akizungumza wakati wa tamasha hilo la TVMC
Afisa Elimu Sayansi Kimu na Afya Manispaa ya Shinyanga,Beatrice Mbonea akizungumza wakati wa tamasha hilo ambapo alilishukuru shirika la TVMC kutoa msaada wa sare za shule na kadi za bima ya afya kwa wanafunzi 200 waliopo katika manispaa ya Shinyanga.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...