Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya CRDB PLC, Dkt. Charles Kimei (wa tatu toka
kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa
CRDB, Tully Mwambapa (wa kwanza kushoto) pamoja Meneja wa Benki ya CRDB
Tawi la Mkwawa Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa
Tawi hilo wakati wa ziara ya Mkurugenzi huyo kutembelea matawi ya nyanda
za juu kusini katika mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya aliyoifanya
mwishoni mwa wiki iliyopita. Picha zote na Cathbert Kajuna -
Kajunason/MMG.
Mkurugenzi
Mtendaji wa CRDB, Dkt. Charles Kimei (kulia) akielekezwa jambo na
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa CRDB, Tully
Mwambapa wakati walipofika katika tawi la Mkwawa -Iringa kujionea
utendaji kazi.
Mkurugenzi
Mtendaji wa CRDB, Dkt. Charles Kimei (kulia) akipata maelezo machache
kutoka kwa meneja wa Tawi la Mkwawa - Iringa Kissa.
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dkt. Charles Kimei akiwaafa wafanyakazi wa Tawi la Mkwawa - Iringa.
Mkuu
wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi
wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa CRDB, Tully Mwambapa (wa pili
kulia) huku akishuhudiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB PLC,
Dkt. Charles Kimei (Kulia) wakati walipofika kumtembelea katika ofisi ya
Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Jamhuri William wakati Dkt. Kimei
alipokuwa ziara katika matawi ya nyanda za Juu Kusini.
Mkuu
wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kulia picha ya juu) akizungumza na
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB PLC, Dkt. Charles Kimei na ujumbe
wake walipofika kumtembelea katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mufindi
Mhe. Jamhuri William wakati Dkt. Kimei alipokuwa ziara katika matawi ya
nyanda za Juu Kusini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...