Na Said Mwishehe,Globu ya Jamii
WATANZANIA ambao wanafanya mazoezi wameshauriwa baada ya kumaliza mazoezi wanywe Yoghurt(maziwa) ya Asas kwani husaidia kulainisha misuli.
Ushauri huo umetolewa na Meneja Masoko wa Infinity Fitness Gym Sia Ndaskoi wakati anazungumzia umuhimu wa kufanya mazoezi sambamba na unywaji wa maziwa ya Asas.
Amesema wanafahamu kuwa baada ya kufanya mazeozi mhusika hupata kiu , hivyo badala ya kunywa maji ni vema akanywa maziwa hayo ambayo kwa sehemu kubwa yatamfanya mwili wake misuli kuachia haraka na kumuondelea maumivu ya mwili.
Amesema mtu anayefanya mazoezi mwili wake unakuwa imara na hausumbuliwi a magonjwa na hivyo ametoa mwito kwa wananchi kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi na kasha wasisahau kunywa maziwa ya Asas.
Ndaskoi ambaye pia amewahi kushiri mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2009 amesema  kwa anayefanya mazoezi inakuwa ngumu kuzeeka mapema , hivyo ushauri wake ni watanzania kujikita kufanya mazoezi ambayo pia husaidia kuondoa mafuta mwilini na hata kwa aliye na msongo wa mawazo akifanya mazoezi yanamsaidia kuuondoa mawazo.
Meneja wa Infinity Fitness Gym Sia Ndaskoi wa Infinity Fitness Gym Sia Ndaskoiwa pili kutoka kushoto akiwa na wafanyakazi wenzake kwenye banda la ASAS kwenye  maonyesho ya biashara ya TANTRADE viwanja vya Sabasaba jijini Dar es salaam leo.
Meneja wa Infinity Fitness Gym Sia Ndaskoi wa Infinity Fitness Gym Sia Ndaskoi wa pili kutoka kushoto akiwa na wafanyakazi wenzake wakionyesha baadhi ya vifaa vya mazoezi kwenye banda la ASAS kwenye  maonyesho ya biashara ya TANTRADE viwanja vya Sabasaba jijini Dar es salaam 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...