Na Karama Kenyunko, blogu ya jami

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali ombi la upande wa utetezi katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema na wenzake saba lililokuwa linatoa taarifa ya kusudio la kukata rufaa dhidi ya uamuzi mdogo uliotolewa mahakamani hapo jana.

Hatua hiyo imekuja baada ya upande wa mashtaka Juni 11mwaka 2018 kuamuriwa na Mahakama wafanye marekebisho katika hati ya mashtaka baada dhidi ya washtakiwa hao badaa ya hati hiyo, kuonekana kuwa na mashtaka batili na yenye mapungufu ya kisheria.

Kutokana na kutupwa kwa kusudio hilo la kukata rufaa, washtakiwa hao wamesomewa mashtaka mapya 13 na na Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...