Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Usafari wa Anga Tanzania (TCAA) Ally Changwila (kushoto) akimfafanulia mmoja wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam, aliyetembelea kwenye banda la Mamlaka hiyo juu ya mikakati ya usafiri wa anga kupunguza uchafuzi wa mazingira, wakati wa maonesho ya Wiki ya Mazingira yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam, waliotembelea kwenye banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania(TCAA) wakimsikilza kwa makini afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Ally Changwila (katikati) wakati akiwafafanulia jambo juu ya mikakati ya usafiri wa anga kupunguza uchafuzi wa mazingira, wakati wa maonesho ya Wiki ya Mazingira yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mnazi Mmoja jijini Dar eS Salaam, waliotembelea katika banda la TCAA, wakimsikiliza kwa makini Mratibu wa mazingira wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) John Mfungo wakati akiwaelezea juu ya mikakati ya usafiri wa anga walivyojipanga kupunguza uchafuzi wa mazingira, wakati wa maonesho ya Wiki ya Mazingira yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...