Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) akisaini Mkataba wa makubaliano ya ushirikiano baina ya Magereza nchini SheliSheli na Jeshi la Magereza Tanzania Bara. Kushoto ni Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli hiyo Raymond St Ange akisaini mkataba huo. Hafla fupi ya utilianaji saini Mkataba huo umefanyika leo Juni, 2018 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dkt. Juma Malewa(kulia) na Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange wakionesha nyaraka za Mkataba wa makubaliano mara baada ya utiliananji wa mkataba huo ambapo Jeshi la Magereza linatarajia kupeleka baadhi ya Maofisa wa Jeshi hilo kwenda nchini SheliSheli kusaidia kuwajengea uwezo wa Uendeshaji wa Magereza nchini humo.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakishuhudia utiliananji saini wa mkataba huo (Kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga(katikati) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila Kushoto ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Charles Novart.
Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange(kushoto) akiwa pamoja na ujumbe wake kabla ya kusainiana Mkataba wa makubaliano hayo,(kulia) ni Balozi wa Heshima wa SheliSheli nchini Tanzania, Maryvonne Pool akifuatilia mazungumzo hayo kama inavyoonekana katika picha.
Mkuu wa Magereza nchini Shelisheli Raymond St Ange pamoja na ujumbe wake na Maofisa wa Jeshi la Magereza wakitembezwa ndani ya Kiwanda cha USeremala Gereza Kuu Ukonga kama inavyoonekana katika picha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...