Na Agness Francis, Globu ya Jamii

MCHEZAJI Donald Ngoma aliyesaini na timu ya Azam FC kwa mwaka mmoja akitoke Yanga SC anatarajiwa kwenda nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu yake.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Msemaji Mkuu wa timu hiyo Jaffary Iddy amesema Ngoma ataambatana na Dk. Mwanandi ambaye ndiye mkuu wa kitengo cha afya Azam FC kuelekea mji wa CaptTown kwa ajili ya matibabu katika Hospitali ya St Parot.

Amefafanua wataondoka ya saa 9:45 usiku wa leo kwa kutumia usafiri wa Shirika la Ndege la Kenya Airways.“Uongozi wa Azam unampeleka mchezaji huyo katika matibabu kwa kuwa wanaamini ana uwezo na atatoa mchango mkubwa katika klabu yetu,”amesema.

Mchezaji huyo raia wa Zimbawe alisajiliwa na matajiri hao wa chamazi akiwa majeru wa muda mrefu mpaka kupelekea kutokufanya vizuri msimu mzima uliopita kwa wajiri wake wa zamani Yanga SC.

Jaffary Iddy amesema Ngoma atafanyiwa matibabu ya vipimo vya afya yake kwa gharama zozote.

"Mchezaji huyu akikutwa na ugonjwa atatibiwa kwa gharama zozote ilimradi apone na kucheza na ikionekana hana tatizo lolote atarudi Dar es salaam kwa ajili ya kuongeza mkataba mnono zaidi na kuitumikia Azam FC kwa muda mrefu katika Ligi Kuu Tanzania Bara,"amesema Jaffary.
Mchezaj Donald Ngoma aikiwa katika Jezi za waajiri wake wa zamani YangasSc.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...