Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo 
 RAIS wa Jamhuri ya Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ametoa kiasi cho dola elfu kumi kwa mkuu wa chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole kilichopo Bagamoyo Mkoani Pwani kwa ajili ya ukarabati. 
 Ametoa kiasi hicho ikiwa kama shukrani yake ambazo amesema zitasaidia kutatua baadhi ya changamoto chuoni hapo. Rais Mnangagwa alisema hayo mapema Juni 29 alipotembelea iliyokuwa shule ya wapigania uhuru wa chama cha FRELIMO ambacho hivi sasa ni Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole kilichopo Bagamoyo . 
 Aidha alieleza endapo kutakuwa na uwezekano ataongeza dola nyingine 50 ili kuongezea kiasi alichotoa kwa ajili ya ukarabati chuoni humo . Akiwa chuoni hapo alisema yeye ni mojawapo ya waanzilishi wa chuo hicho katika miaka ya sitini akiwa pamoja na viongozi wengine wa Chama cha FRELIMO . 
 Alisema kwamba alikuwa kiongozi wa ulinzi wa chuo hicho na hawakuwa na dhumuni la kutafuta madaraka bali ilikuwa ni jitihada zilizosukumwa na uzalendo wa kuzipatia nchi zao uhuru. Rais Mnangagwa alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa fursa ya kuitembelea Shule hiyo kwa kuwa ilikuwa ni shauku yake baada ya kuondoka shuleni hapo miaka 58 iliyopita . 
 "Nimefarijika kutembelea Bagamoyo na kuja Tanzania naamini mwaliko huu utaendeleza mahusiano ya nchi hizi uliokuwepo kipindi kirefu" alibainisha.
 Aliwashukuru wananchi wa eneo hilo kwa kumtunza katika kipindi chote alichoishi Bagamoyo hata sasa anajisikia kuwa ni mmojawapo wa jamii ya watu wa wilaya hiyo. Rais huyo aliingia Tanzania Juni 28 ambapo alisema Tanzania na Zimbabwe wataendelea kuimarisha ushirikiano wao.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Edmund Mndolwa mara baada ya kuwasili katika chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani. Rais huyo wa Zimbabwe alisoma Shuleni hapo mwaka 1963 pamoja na wapigani Uhuru wa Chama cha FRELIMO na ilijulikana kama Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya  wapigania Uhuru wa Chama cha FRELIMO.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akizungumza na wafanyakazi pamoja na wanafunzi wanaosoma katika Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole ambapo miaka ya nyuma alisoma hapo wakati huo ikijulikana kama Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya wapigani Uhuru ya Chama cha FRELIMO.
 Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akiangalia moja ya sufuria waliokuwa wakiitumia katika matumizi yao ya kila siku  wakati wakisoma katika Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya wapigani Uhuru ya Chama cha FRELIMO.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akiwa katika picha na Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Edmund Mndolwa, Viongozi wengine wa Tanzania na Zimbabwe pamoja na wanafunzi wanaosoma katika chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo wakati alipokuwa akielekea katika moja ya madarasa ambayo walikuwa wakiyatumia kuanzia mwaka 1963.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akitoka katika moja ya mabweni waliyoyatumia katika mwaka 1963 wakatika wakiwa katika Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya wapigani Uhuru ya Chama cha FRELIMO ambacho sasa kina julikana kama chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani.
 Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi mara baada ya kumaliza kukagua baadhi ya madarasa na mabweni waliyokuwa wakiyatumia katika Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya wapigani Uhuru ya Chama cha FRELIMO ambacho sasa kinajulikana kama chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani.
 Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akipunga mkono kwa kikundi cha ngoma za asili wakati akiondoka katika eneo la chuo hicho cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani. 
PICHA NA IKULU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...