Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 
 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe amemuagiza mkuu wa Kituo Cha Polisi Gairo kuwakamata wale wote waliokula fedha za ujenzi wa maabara ya shule sekondari ya Idibo iliyiyopo katika Kata ya Idibo wilayani Gairo. 
 Akizungumza katika mkutano wa hadhara hizi karibuni Dkt. Dkt. Kebwe Stephen Kebwe amesema kuwa hawezi kuvumilia kuona shilingi Milioni 12 fedha za ujenzi wa maabara zilizotokana na nguvu ya wananchi zinaliwa na watu wachache tena bila kufanikisha malengo. 
"Hivi kuna watu bado hawaelewi umuhimu wa kutunza fedha za umma??? Haiwezekani wananchi wajichange harafu nyie viongozi wa kijiji mle hela zao za maendeleo bila aibu, siwezi kuvumilia... Nakuagiza OCD Gairo na TAKUKURU kufanya msako watu hawa wapelekwe mbele ya sheria haijalishi walishastaafu au la!," amesema.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe (Katikati) akiwahutubia wakati kijiji cha Chakwale mara baada ya kufanya usafi katika Soko la Chakwale katika ziara yake aliyoifanya hivi karibuni kwa ajili ya kuhamasisha miradi ya maendeleo wiyani humo. 
.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe (wa tano toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Wilaya ya Gairo ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe (kulia kwake), Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Gairo, Agnes Mkandya, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Rachel Nyangasi (wa kulia kwa mkuu wa mkoa) pamoja na wengine. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akipokea zawadi ya mahindi mara baada ya kuwahutubia (katikati) wananchi wa kijiji cha Chakwale mara baada ya kufanya usafi katika Soko la Chakwale katika ziara yake aliyoifanya hivi karibuni kwa ajili ya kuhamasisha miradi ya maendeleo wiyani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akisikiliza maelezo mafupi ya ujenzi wa shule ya Idibo ulioanza mwaka 2014 ambapo mpaka sasa ujenzi wake umekwama katika ziara yake aliyoifanya hivi karibuni kwa ajili ya kuhamasisha miradi ya maendeleo wiyani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe (mwenye kofia) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe (mwenye kilemba), Diwani Kata ya Idibo Mhe. Rajabu Mguhi pamoja na pamoja na viongozi wengine wa Wilaya ya kijiji wakiwa katika ziara kwa ajili ya kuhamasisha miradi ya maendeleo wiyani humo. Habari  kamili BOFYA HAPA



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...