SERIKALI imeanza kulishughulikia tatizo la maji wilayani Muheza kwa vitendo baada ya kutoa kiasi cha bilioni 40 kwa ajili ya kutoa maji kwenye chanzo cha mto zigi kupelekwa kwenye vijiji mbalimbali ili kuweza kuondosha kero hizo iliyokuwepo muda mrefu iliyokuwa ikiwafanya wananchi kutumia muda mwingi kusaka huduma hiyo.

Hayo yalibainishwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isaack Kamwele wakati alipofanya ziara wilayani humo kutembelea vyanzo vya maji Amani na kuzungumza na wananchi katika Kijiji cha Mashewa Tarafa ya Amani.

Alisema kuwa mpango huo wa serikali unakusudia kuhakikisha changamoto za maji ambazo walikuwa wanakabiliana nazo wananchi hao kwa muda mrefu zinamaliza ili waweze kunufaika na huduma hiyo muhimu kwa ustawi wa maisha yao na jamii zinazowazunguka.

Waziri Kamwelwe alisema hatua hiyo ni juhudi kubwa zinazofanywa na Rais John Magufuli kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi zikiwemo za maji ili kuhakikisha tatizo la kutokupatikana kwa huduma hiyo linaondoka kwa watanzania.

“Ndugu zangu serikali tumetoa bilioni 40 kwa ajili ya kushughulikia tatizo la maji wilayani Muheza kutoka chanzo cha Mto zigi kupita vijiji vyote hadi Muheza mjini huu ni mpango wa kuhakikisha changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji Muheza tunaipatia ufumbuzi wa kina “Alisema.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe kushoto akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella wakitazama namna maji yanavyotoka kwenye Kijiji cha Mashewa Tarafa ya Amani wakati alipofanya ziara kutembelea vyanzo vya maji kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi
 Mkandarasi anayetekeleza mradi wa maji kutoka Pongwe hadi Jijini Tanga kutoka kampuni ya Koberg Contrustion Co.Limited Stephen Kingili wa pili kulia akimuonyesha jambo Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe kushoto wakati alipotembelea na kuangalia tanki kubwa la maji eneo la Ngomeni wilayani Muheza ambalo litakalokuwa la lita milioni saba  linalotarajiwa kukamilika mwezi wa tatu mwakani litakuwa limekamilika kwa ajili ya kutoa maji Pongwe Jijini Tanga hadi wilayani Muheza
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe akisisitiza kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe akiangalia mchanga unazotumika kwenye ujenzi wa tanki la maji eneo la Ngomeni
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe akiangalia kikoto  zinazotumika kwenye ujenzi wa tanki la maji eneo la Ngomeni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...