SERIKALI
imeutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kuongeza kasi katika
kubuni mikakati na maboresho ikiwemo taratibu za kujiunga ambazo
zitawawezesha wananchi wengi zaidi kunufaika na huduma zake.
Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akizindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa NHIF mjini Morogoro ambapo amesema kuwa mwelekeo wa Serikali kwa sasa ni kuhakikisha watu wote wanakuwa na bima ya afya.
"Serikali ya Awamu ya Tano imeweka nguvu kubwa katika utoaji wa huduma bora za matibabu kwa wananchi hivyo ninawaagiza muongeze kasi katika ubunifu na maboresho mbalimbali ambayo yatakwenda sambamba na matarajio ya Serikali yanayolenga wananchi wengi zaidi kuwa katika mfumo wa kupata huduma za matibabu kwa mfumo wa bima ya afya,” amesema Dk. Ndugulile.
Amewataka watumishi wa Mfuko hususan Mameneja wa Mikoa kutokaa maofisini mwao na badala yake watoke nje kwa ajili ya kuhamasisha wananchi, kuangalia huduma wanazopata katika vituo vya kutolea huduma pamoja na kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika maeneo mbalimbali.
Akizungumzia utendaji kazi wa Baraza, amewataka wajumbe wa baraza hilo kutambua wajibu wao ndani ya baraza kwa kuwa ni chombo muhimu katika kubuni na kuweka mipango thabiti ya kuendesha taasisi ambayo ina dhamana kubwa ya kuangalia ama kushughulikia huduma za matibabu kwa wanachama.
Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akizindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa NHIF mjini Morogoro ambapo amesema kuwa mwelekeo wa Serikali kwa sasa ni kuhakikisha watu wote wanakuwa na bima ya afya.
"Serikali ya Awamu ya Tano imeweka nguvu kubwa katika utoaji wa huduma bora za matibabu kwa wananchi hivyo ninawaagiza muongeze kasi katika ubunifu na maboresho mbalimbali ambayo yatakwenda sambamba na matarajio ya Serikali yanayolenga wananchi wengi zaidi kuwa katika mfumo wa kupata huduma za matibabu kwa mfumo wa bima ya afya,” amesema Dk. Ndugulile.
Amewataka watumishi wa Mfuko hususan Mameneja wa Mikoa kutokaa maofisini mwao na badala yake watoke nje kwa ajili ya kuhamasisha wananchi, kuangalia huduma wanazopata katika vituo vya kutolea huduma pamoja na kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika maeneo mbalimbali.
Akizungumzia utendaji kazi wa Baraza, amewataka wajumbe wa baraza hilo kutambua wajibu wao ndani ya baraza kwa kuwa ni chombo muhimu katika kubuni na kuweka mipango thabiti ya kuendesha taasisi ambayo ina dhamana kubwa ya kuangalia ama kushughulikia huduma za matibabu kwa wanachama.
Naibu
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine
Ndugulile akizindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa
Bima ya Afya (NHIF), mkoani Morogoro.
Naibu
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine
Ndugulile akimkabidhi nyaraka za kuongoza Baraza hilo, Mkurugenzi Mkuu
wa NHIF, Bernard Konga.
Wajumbe wa Baraza la Pili la NHIF, wakionyesha ishara ya mshikamano baada ya kuzinduliwa rasmi kwa Baraza hilo.
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza wakionyesha ishara ya mshikamano.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...