Na Agness Francis, Globu ya Jamii.
King Cash and Isbah Entertainment inawaletea burudani kabambe wakazi wa kanda ya Ziwa Tamasha la Sports Music Festival 2018 katika kusherehekea sikuku ya Idd.
Tamasha hilo la aina yake litakalosindikizwa na wasanii mbalimbali wa bongo fleva hapa nchini.
Wasanii hao watakao tumbuiza siku hizo ni Mbunge wa Mikumi Profesa Jay, Juma Nature, Young Killer, Roma, Stamina, Fid Q, Bill Nas, Umber Lulu, Snura, Msaga Sumu, G Nako, Young Dee, Coyo Mc, Fany, B-Gwai pamoja na mkali wa singeli Shalo Mwamba.
Siku ya Idd Mosi wataanzia Geita katika viwanjwa vya Infotech ambapo kiingilio kwa wakubwa ni shilingi 5000 na watoto ni 3000.
Ambapo Idd pili watatapiga hodi Mkoani Mwanza katika viwanja vya CCM kirumba,na baada ya hapo watamalizia burudani Mjini Kahama pale Uwanja wa Taifa kwa kiingilio cha Shilingi 10000 wakubwa,huki watoto wakilipia mlangoni 5000.
Tamasha hilo litaanza saa 4 asubuhi mpaka majogoo ambapo pia watashuhudia michezo ya piki piki na magari yakifanya maajabu yake ya dunia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...