Bw. Ally M. Koyya, (kulia), kutoka idara ya Masoko TANESCO, akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea kwenye banda la Shirika hilo kwenye maonesho ya Nishati Mbadala yanayokwenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Juni 4, 2018.
NA
K-VIS BLOG/Khalfan Said
SHIRIKA
la Umeme Nchini (TANESCO) limesema hakuna sababu yoyote kwa wananchi kuogopa
kutumia nishati ya umeme kwa matumizi mbalimbali ya nyumbani kwani ni nafuu mno
ukilinganisha na nishati nyingine.
Afisa
Mazingira wa Shirika hilo, Bw.Yusuf Kamote, amesema hayo kwenye maonesho ya
Nishati mbadala ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yanayoendelea
kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Juni 4, 2018, ambapo
kauli mbiu ya mwaka huu ni “Mkaa ni ghali
tutumie Nishati mbadala”.
“Siku
zote tunasema umeme wa TANESCO ni umeme wa bei nafuu, jambo la msingi ambalo
wananchi wanapaswa kuelewa ni matumizi sahihi ya vifaa vya umeme kulingana na
mahitaji.” Alisema.
Alisema
kwa mfano mtu anatumia kifaa kinachohitaji WATI
100 (100watts) kwa saa moja lakini anatumia kifaa cha WATI 200 (200Watts) kwa saa na kwa mahitaji yanayofanana, bila
shaka hayo sio matumizi bora ya umeme.
Wanafunzi wa shule ya sekondari Kanosa ya jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya kitaalamu na wataalamu wa TANESCO (Kushoto).
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...