Angela Msimbira OR-TAMISEMI


Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Joseph Kandege  amewaagiza wafugaji nchini kuunda  vyama vya ushirika imara ambavyo vitawezesha  kupata huduma za mifugo na kuboresha ukusanyaji na masoko ya maziwa. 



Mhe Kandege ameyasema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Maziwa iliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Nanenane, Themi Mkoani Arusha Mhe. Kandege amesema uwepo wa ushirika imara utaboresha ukusanyaji wa  maziwa kwa wingi kwa ufanisi zaidi na hatimaye  kuongeza kiasi cha usindikaji kwa viwanda. 



“Napenda kutoa pongezi kwa wafugaji wa Mikoa ya Tanga na Njombe kwa kuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa mafanikio yanayoonekana katika kuendeleza tasnia ya maziwa kupitia ushirika” Amesema Kandege.Amesisistiza kuwa Mamlaka za Serikali za Mitaa na idara zake nchini kuhakikisha zinawezesha uundwaji wa vyama vya ushirika imara na pia wanaimarisha vyama vya ushirika vilivyopo.

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Joseph Kandege akikagua moja ya machine inayotumika katika usindikaji wa maziwa kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki ya maziwa kilichofanyika leo katika viwanja Nanenane Themi, Mkoani Arusha.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Joseph Kandege akikabidhiwa maziwa kwa ajili ya shule mbalimbali katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya maziwa kilichofanyika leo katika viwanja Nanenane Themi, Mkoani Arusha.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Joseph Kandege akiwa na baadhi ya viongozi wakati akitembelea mabanda ya maonyesho kwenye  kilele cha maadhimisho ya wiki ya maziwa kilichofanyika leo katika viwanja Nanenane Themi, Mkoani Arusha.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Joseph Kandege akiongea na wadau wa ufugaji katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya maziwa kilichofanyika leo katika viwanja Nanenane Themi, Mkoani Arusha.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...