
Wakata miwa wa Morogoro Mtibwa Sugar wamefanikiwa kunyakua ubingwa wa mashindano ya Azam Sports Federation Cup 2018 baada ya kuifunga Singida United.
Mtibwa imewachukua miaka 18 kunyakua ubingwa baada ya mara ya mwisho mwaka 2000 walipotawazwa ubingwa wa ligi kuu.
Mtibwa Sugar imefanikiwa kutwaa taji hilo la Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Singida United. .
Mtibwa imewachukua miaka 18 kuchukua ubingwa kwa kuwafunga Singida United magoli matatu kwa mawili huku magoli ya Mtibwa sugar yakifungwa na Salum kihimbwa dk 22, Issa Rashidi dk 37 na Ismail mhesa dk ya 90 huku magoli ya Singida United yakifungwa na Chuku dk ya 43 na Kutinyu dk ya 71.



Picha na Mwaisabula.blogspot
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...