Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii

WALINZI 10 wa kampuni ya ulinzi  ya KK na muendesha foko mmoja wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kula njama na wizi wa mapipa 26 ya makinikia ya madini yenye thamani ya Sh. 1,705,296,434.4.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri, wakili wa Serikali, Patrick Mwita amewataja washtakiwa hao kuwa ni Omar Omar (24), Boniface Mahingu (44), Haji Chalaza (30), Fadhil Kilima (28), Paulo Bigambo (27), Mwema Bakari (37), Israel Yeckonia (31), Steven Kamala(35), Adam Brarugaba(32), Loshiru Lukumay(32) wote walinzi wa KK na Albert Mbaga(34) ambaye ni muendesha foko.
 Imedaiwa Aprili 21 mwaka 2018 jijini  Dar es salaam washtakiwa kwa pamoja wakiwa na wenzao ambao hawapo mahakamani walikula njama ya kutenda kosa la wizi.

Wakili Mwita alidai siku hiyo ya katika eneo la Tabata Relini  wilaya ya Ilala washtakiwa hao kwa pamoja huku wakijua kuwa ni  makosa na kinyume cha sheria waliiba mapipa 26 ya makinikia ya madini ya Tuntulum yenye thamani ya Sh 1,705,296,434.4 mali ya kampuni ya Ballore Logistics.

Hata hivyo, washtakiwa hao wamekanusha mashtaka yote hayo na wamerudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Washtakiwa hao wametakiwa kutoa sh. Milioni 78 ama awasilishe hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.

Pia kila mshtakiwa anatakiwa kuwa na wadhamini wawili ambapo kila mdhamini atasaini bondi ya sh milioni 50. Wadhamini hao, pia wametakiwa kuwa na utambulisho wa barua na nakala za vitambulisho vyao halali, kisha  washtakiwa wameambiwa hawaruhusiwi kutoka  nje ya jiji la Dar es Salaam bila ya kuwa na kibali cha mahakama.
 Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 14 mwaka 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...