Na.Vero Ignatus Arusha.

Imeelezwa kuwa kuandaa wosia mapema kabla ya kifo inasaidia kuepuka mogogoro ya mirathi ambayo imekuwa ikiwakumba wajane.

Hayo yamesemwa na Naibu meya wa jiji la Arusha Viola Lazaro katika maadhimisho ya siku ya wajane duniani mkoani iliyofanyika Palace Hotel Mkoani Arusha.Akitoa changamoto wanazo pitia wajane Bi Janet Mgane amesema matatizo ya Mirathi, Wajane kushindwa kufahamu sheria na kesi kuchukua muda Mrefu.

Akijibu risala iliyosomwa na mratibu wa tawia Kanda ya KaskaziniJuliet Mgani, Naibu meya amesema changamoto kubwa waliyonayo ni wanawake wengi kutokuzifahamu haki zao kisheria na kikariba."Wanawake wengi amabao ni wajane wanashindwa kupambana kushinda kesi kwa kutokufahamu sheria na kikatiba" Alisema naibu meya.Mmoja wa wajane bi Agness Omari (78)ametoa ushauri kwa wajane wajiheshimu na kuwalea watoto walioachiwa na waume zao waliotangulia mbele za haki.

Kauli mbiu ya siku ya wajane duniani "wajane tusibaki nyuma katika kuelekea uchumi wa viwanda na malengo ya maendeleo endelevu 2030.

Naibu Meya wa Jijila Arusha Viola Lazaro akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wajane duniani yaliyoyanyika katika Hotel ya Palace mkoani Arusha ambapo alikuwa mgeni rasmi.Picha na Vero Ignatus 
Mratibu wa chama cha wanawake wajane Jijini Arusha(TAWIA) bi Janet Mgane akisoma risala mbele ya mgeni rasmipamoja na wanawake wajane waliohuduria katika kuadhimisha siku yao mkoani Arusha ambapo zaidi ya wanwake 50 waliwezakuhudhuria huku ikiwa ni mara yao ya kwanza kuadhimishwa mkoani hapo.Picha na Vero Ignatus .
Wakwanza kulia ni Mratibu wa chama cha wanawake wajane mkoani Arusha bi Janet Mgane,akimkabidhi mgeni rasmi risala Naibu meya wa jiji la Arusha Viola Lazaro,katikati ni diwani wa viti maalum chadema Happy Charles akufuatiwa na Mkurugenzi wa jinsia na mahusiano ya jamii kutoka shirika la Civil and Legal Aid Organization Ranto Muhochi.Picha na Vero Ignatus
Diwani wa viti maalum chadema Happy Charles akizungumza na wanawake wajane katika ukumbi wa Hotel ya Palace Jijini Arusha. 
Meneja wa Biashara kutoka Benki ya CRDB Rose Wilium akizungumza na wanawake wajane akiwaelekeza namna ya kufungua akaunti na namana ya kujikwamua kiuchumi. Picha na Vero Ignatus 
Pichani ni baadhi ya wanawake wajane (TAWIA)pamoja na baadhi ya viongozi wa chama cha wanawake wajane nchini,wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Naibu Meya wa Jiji la Arusha Viola Lazaro.Picha na Vero Ignatus 
Baadhi ya waandishi wa habari Mkoani Arusha walioalikwa kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyika kimkoa katika Hotel ya Palace.Picha na Vero Ignatus 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...