Kampuni ya simu za mkononi inayoongoza kwa utoaji wa huduma bora za Smartphone Airtel Tanzania kupitia huduma yake ya Airtel Money leo imetangaza na kuzindua huduma mpya kwa wateja wote wanaotumia huduma ya kutuma na kupokea pesa kupitia Airtel Money kwa sasa wataweza kutuma na kupokea pesa bure bila ya makato yoyote.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam kwa niamba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Isack Nchunda alisema, “Tunayo furaha kubwa kuona ungezeko la watumiaji wa Airtel Money kila siku, tunaamini ya kuwa malengo ya serikali ya kuhakikisha inafanikisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa kila mwananchi linaelekea kupata mafanikio makubwa. Leo Airtel tunazindua huduma hii inayojulikana kama HAKATWI MTU HAPA – Tuma Pesa Bure ili kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali na kuwawezesha wateja wetu zaidi ya milioni 10 nchini kuweza kutuma na kupokea Pesa BURE”.

“Mwaka jana Airtel tulizindua huduma ya ya kutuma na kupokea pesa bure kwa wateja wa Airtel Money wanaotuma pesa kuanzia 200,000 na kuendelea. Tumezingatia tena uhitaji wa wateja wetu wengi hivyo kupitia HAKATWI MTU-Tuma Pesa Bure tunaamini wale wanaotuma pesa chini ya hapo wataweza kufurahia huduma hii ya Bure.

 Ni imani yetu kwamba huduma ya tuma na pokea pesa bure kupitia Airtel Money itakuwa ni chachu kwa wale ambao sio wateja wa Airtel Money kuanza kutumia huduma hii salama, rahisi na ya uhakika,  Tunategemea kuona wateja wakichangamkia  Fursa hii ya kutuma na kupokea pesa bila makato yoyote ili  kuokoa pesa  hadi Sh 5,000 kuanzia sasa”. alieleza Nchunda
Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Isack Nchunda akiongea wakati wa kuzindua huduma inayojulikana kama HAKATWI MTU HAPA – Tuma Pesa Bure ambapo wateja wote wanaotumia huduma ya kutuma na kupokea pesa kupitia Airtel Money kwa sasa wataweza kutuma na kupokea pesa bure bila ya makato yoyote kwa kupinga *150*60# kisha changua tuma pesa bure.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano akiongea wakati wa kuzindua huduma inayojulikana kama HAKATWI MTU HAPA – Tuma Pesa Bure ambapo wateja wote wanaotumia huduma ya kutuma na kupokea pesa kupitia Airtel Money kwa sasa wataweza kutuma na kupokea pesa bure bila ya makato yoyote kwa kupinga *150*60# kisha changua tuma pesa bure.
Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Isack Nchunda – kulia na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni wakionyesha bango baada kuzindua huduma inayojulikana kama HAKATWI MTU HAPA – Tuma Pesa Bure ambapo wateja wote wanaotumia huduma ya kutuma na kupokea pesa kupitia Airtel Money kwa sasa wataweza kutuma na kupokea pesa bure bila ya makato yoyote kwa kupinga *150*60# kisha changua tuma pesa bure.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...