Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Benki ya KCB Tanzania imefanya uzinduzi wa tawi lake la 14 lililopo Mbagala jijini Dar es salaam. Tawi hilo limezinduliwa rasmi na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mh. Dkt Ashatu Kijaji akiwa ameambatana na Mbunge wa Mbagala Issa Mangungu.
Dkt Ashatu amesema kuwa amefurahishwa na utendaji kazi wa benki ya DCB ndani ya miaka mitano ikiwemo ulipaji wa kodi na jumla ya Bilioni 40 imelipwa kama kama cooperate Tax na kodi nyinginezo.
Amesema kuwa KCB imeshirikiana na serikali katika utekelezaji wa miradi ikiwemo ujenzi wa barabara na majengo mbalimbali, udhamini waligi kuu ya soka Tanzania ikiwa ni lengo la kuinua sekta ya michezo.
Katika uzinduzi huu Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Zuhura Muro aliweza kusena baadhi ya mafanikio machache ambayo KCB imeweza kufanya kwa jamii.

Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji akikata utepe baada ya
kuzindua tawi la Benki ya KCB Mbagala leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji akizindua tawi la Benki ya
KCB Mbagala akiwa pamojpana Mkurugenzi Mtendaji Cosmas Kimaro na
Mwenyekiti wa Bodi Zuhura Muro leo Jijini Dar es Salaam.

Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji akizungumza na wananchi
waliojitokeza pamoja na viongozi wa Benki ya KCB wakati wa uzinduzi wa
tawi la Mbagala Leo Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki KCB Zuhura Muro akizungumza wakati wa uzinduzi wa tawi la Benki hiyo Mbagala leo Jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...