Na Said Mwishehe Blogu ya Jamii
CHUO cha Kodi (ITA) kimesema kwa sasa kimeanza kupokea maombi ya wanaotaka kujiunga na chuo hicho kwa mwaka wa masomo wa 2018/2019 na kwamba wamekuwa wakielezea program ambazo wanazitoa.
Pia kimesema wanafunzi wote wenye sifa watume maombi kwa kozi ambazo wanahitaji kusoma na kwamba wanaosoa chuoni hapo na kumaliza wanaweza kufanya kazi mahali popote kwa kuajiriwa au kujiajiri.
Akizungumza na Michuzi Blog leo katika Banda la Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) ambako ndani yake kuna banda la Chuo cha Kodi Mkuu wa Mawasiliano wa chuo hicho Oliver Njunwa amesema wanaombaji watumie maombi kwa njia ya mtandao kupitia www.ita.ac.tz au http://212.71.252.209/ita-oas/.
Ametaja kozi ambazo zinatolewa na chuo hicho ni Astashahada ya Forodha na Usimamizi wa kodi na Stashahada ya Forodha na Usimamizi wa Kodi.
Pia Shahada ya Forodha na Usimamizi wa kodi, Stashahada ya Uzamili wa Usimamizi wa kodi, Cheti Afrika Mashariki cha Uwakala wa Forodha pamoja na Shahada ya Uzamili ya Sheria ya kodi na usimamizi.
Alipoulizwa ni kitu gani hasa ambacho wanakifanya katika maonesho hayo, amejibu kuwa wanatumia maonesho hayo kwa ajili ya kuzungumza na watanzania kuhusu uwepo wa chuo hicho na faida zake na kubwa ni kuwahamasisha kujiunga na chuo hicho.
“Chuo cha Kodi ni chuo pekee kwa nchi za ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini katika utoaji wa mafunzo ya forodha na kodi.
“Chuo chetu kinatoa mafunzo kwa wadau mbalimbali na hiyo imetufanya tupokee wanafunzi kutoka nchi nyingi za Afrika,”amesema Njunwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...