Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema hakitashiriki Uchaguzi mdogo wa marudio katika Kata 79 na majimbo mawili ambao umetengazwa kufanyika Agosti 12 mwaka huu.
Taarifa ya Naibu Mkurugenzi wa habari, Uenezi na Uhusiano na Umma Mbarala Maharagande ametoa taarifa ya kutoshiriki kwenye uchaguzi kwa vyombo vya habari na kufafanua uamuzi huo umetokana na Kamati ya Utendaji baada ya kufanya uchambuzi na tathimini ya kina kuhusu tangazo la kufanyika uchaguzi huo.
Maragande ambaye yeye anatoka CUF ya upande wa Katibu Mkuu wa chama hicho Maalim Seif Ahmad amesema sababu za msingi za kutoshiriki katika uchaguzi huo ni nyingi moja wapo ikiwa ni mgawanyiko wa uongozi Katika uchaguzi huo uliojitokeza kutokana na mgogoro aliodai umepandakizwa na Profesa Ibrahim Lipumba na Washiriki wake
Hivyo amesema CUF unaona ni ishara kwa sasa kuelekeza nguvu na rasilimali zake chache zilizopo katika kushughulika na kupata ufumbuzi wa mgogoro uliopo. Ameongeza kuwa CUF inatoa mwito kwa vyama rafiki vyote katika UKAWA kukaa pamoja kufikia muafaka na maridhiano na kusimamisha wagombea bora, imara, na madhubuti kugombea nafasi hizo zote.
"CUF inatoa mwito kwa viongozi na wanachama wake wote katika maeneo yote ya marejeo ya uchaguzi kwa Tanzania Bara kushirikiana bega kwa bega na kuunganisha nguvu za pamoja na vyama rafiki vya UKAWA katika uchaguzi huu ili kuishinda CCM,"amesema.
Maharagande amesema katikankata 79 zilizotangazwa, CUF imepoteza Kata 4 ilizokuwa inaziongoza kwa madiwani wake ambao waliamua kwenda CCM. Kata mbili zipo manispaa ya Jiji la Tanga Mjini na Kata moja Mtwara Vijijini na Diwani mmoja Kufariki (Wilaya ya Kwimba).
Kutokana na vigezo vya kitaalamu na kitakwimu na ramani ya maeneo utakapofanyika uchaguzi huo wa marudio CUF ingeweza kushiriki kikamilifu katika Kata za mkakati 11 pekee.
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema hakitashiriki Uchaguzi mdogo wa marudio katika Kata 79 na majimbo mawili ambao umetengazwa kufanyika Agosti 12 mwaka huu.
Taarifa ya Naibu Mkurugenzi wa habari, Uenezi na Uhusiano na Umma Mbarala Maharagande ametoa taarifa ya kutoshiriki kwenye uchaguzi kwa vyombo vya habari na kufafanua uamuzi huo umetokana na Kamati ya Utendaji baada ya kufanya uchambuzi na tathimini ya kina kuhusu tangazo la kufanyika uchaguzi huo.
Maragande ambaye yeye anatoka CUF ya upande wa Katibu Mkuu wa chama hicho Maalim Seif Ahmad amesema sababu za msingi za kutoshiriki katika uchaguzi huo ni nyingi moja wapo ikiwa ni mgawanyiko wa uongozi Katika uchaguzi huo uliojitokeza kutokana na mgogoro aliodai umepandakizwa na Profesa Ibrahim Lipumba na Washiriki wake
Hivyo amesema CUF unaona ni ishara kwa sasa kuelekeza nguvu na rasilimali zake chache zilizopo katika kushughulika na kupata ufumbuzi wa mgogoro uliopo. Ameongeza kuwa CUF inatoa mwito kwa vyama rafiki vyote katika UKAWA kukaa pamoja kufikia muafaka na maridhiano na kusimamisha wagombea bora, imara, na madhubuti kugombea nafasi hizo zote.
"CUF inatoa mwito kwa viongozi na wanachama wake wote katika maeneo yote ya marejeo ya uchaguzi kwa Tanzania Bara kushirikiana bega kwa bega na kuunganisha nguvu za pamoja na vyama rafiki vya UKAWA katika uchaguzi huu ili kuishinda CCM,"amesema.
Maharagande amesema katikankata 79 zilizotangazwa, CUF imepoteza Kata 4 ilizokuwa inaziongoza kwa madiwani wake ambao waliamua kwenda CCM. Kata mbili zipo manispaa ya Jiji la Tanga Mjini na Kata moja Mtwara Vijijini na Diwani mmoja Kufariki (Wilaya ya Kwimba).
Kutokana na vigezo vya kitaalamu na kitakwimu na ramani ya maeneo utakapofanyika uchaguzi huo wa marudio CUF ingeweza kushiriki kikamilifu katika Kata za mkakati 11 pekee.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...