Waratibu elimu Kata wameishukuru serikali kwa kuwapatia pikipiki ambazo zitawawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa.
Pikipiki hizo walizopatiwa waratibu hao ni miongoni mwa pikipiki zilizotolewa na serikali kwa waratibu elimu wa Kata zote hapa nchini zenye lengo la kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa waratibu hao.
Waratibu hao wametoa pongezi zao mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo alipokuwa akikabidhi pikipiki 17 kwa waratibu elimu wote wa wilaya hiyo ya kisarawe. Waratibu hao wamemuahidi waziri huyo kwamba watafanya makubwa katika elimu kwa kuwa pikipiki hizo zitawasaidia zoezi la uratibu wa elimu katika kata zao.
Kwa upande wake, Waziri Jafo amewaasa waratibu hao kuzitumia pikipiki hizo kwa lengo la kupandisha taaluma katika maeneo yao. "Ikumbukwe kwamba serikali imekuwa na utaratibu wa kutoa posho ya madaraka kwa waratibu elimu kata pamoja na wakuu wa shule za msingi na serikali hapa nchini,"amesema.Amebainisha kuwa kupatikana kwa pikipiki hizo kutawezesha kuongeza ufaulu kwa wanafunzi hapa nchini.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Seleman Jafo akizungumza na waratibu wa elimu kata ya Kisarawe.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Seleman Jafo akikabidhi pikipiki kwa waratibu kata ya Kisarawe.
Baadhi ya pikipiki za waratibu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Seleman Jafo akikabidhi pikipiki kwa waratibu wa elimu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...