Na Karama Kenyunko, blogu ya Jamii.
Mamlaka ya maji safi na maji taka (Dawasa) inatekeleza mradi Mkubwa wa upanuzi wa chanzo cha maji Chalinze ili kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa maji kwa wakazi wa mkoa wa pwani.
Mradi huo ambao kwa sasa uko katika hatua ya tatu utahakikisha pia upatikanaji wa maji katika viwanda unakuwa wa uhakika.
Akiongea katika ziara ya kukagua.. Maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maji na upanuzi wa chanzo cha mtandao wa maji Chakinze, waziri wa maji na umwagiliaji, Profess Makame Mbarawa.amewahakikishia wawekezaji nchini kuwa jitahada kubwa zinafanywa kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa maji katika viwanda vyote kikiwemo cha Sayona.
Amesema, Dawasa kama sekta ya maji, watahakikisha wanatekeleza azma ya kumaliza tatizo kubwa la maji hadi kwenye viwanda, kwani hakuna kiwanda kitakachoendelea bila ya kuwa na maji ya kutosha.
Naomba niwahakikishie watanzania wenzangu ambao wanania thabiti ya kujenga viwanda kwa ajili ya kukuza uchumi wetu, sisi kama sekta ya maji tutahakikisha kwamba tunawapa nguvu zetu zote na kuwawekea miundombinu ya kisasa ili huduma ya maji iweze kuwafikia na waweze kufanya kazi zao za uzalishaji ili nchi yetu iweze kukua kufikia uchumi wa wakati 2025" amesema Mbarawa.
Waziri
wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa, akizungumza na
watumishi wa Chaliwasa, wilaya ya Chalinze mkoani Pwani kabla ya kukagua
mradi wa uboreshaji upatikanaji Maji Chalinze.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa akiangalia mchoro wa ramani ya mradi huo, Chalinze.

Waziri
wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa, akikagua mradi wa
uboreshaji miundombinu ya maji , Chalinze mkoani Pwani.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa akitoa maagizo
kwa mkandarasi OIA Overseas Infrustrature Alliance mara baada ya
kumaliza ya kukagua mradi wa uboreshaji upatikanaji Maji Chalinze.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...