SHIRIKA
la Taifa la Hafadhi ya Jamii (NSSF) wameshauriwa kutumia Maonesho ya 42
ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya
Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaa
kuhamasisha wanaume wanaofika katika maonesho hayo kupima Virusi vya
Ugonjwa wa UKIMWI (VVU).
Ushauri huo umetolewa leo na Waziri wa Sera, Kazi, Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama, wakati anazungumza na uongozi pamoja na wafanyakazi wa NSSF baada ya kutembelea banda la shirika hilo ili kujionea shughuli ambazo zinatekelezwa na shirika hilo.
Ushauri huo umetolewa leo na Waziri wa Sera, Kazi, Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama, wakati anazungumza na uongozi pamoja na wafanyakazi wa NSSF baada ya kutembelea banda la shirika hilo ili kujionea shughuli ambazo zinatekelezwa na shirika hilo.
Waziri Mhagama pamoja na kutoa pongezi kwa NSSF kutokana na juhudi
ambazo wanazifanya katika kuwahudumia Watanzania pamoja na kuunga mkono
juhudi za ujenzi wa viwanda nchini kwa kujenga kiwanda cha sukari
kilichopo Mbigili mkoani Morogoro ni vema wakaweka dirisha kwa ajili ya
kuhamasisha wananchi kupima Vrusi vya UKIMWI.
“Niwapongeza NSSF kwa kazi nzuri ambayo mnaifanya nchini. Hata hivyo nitoe rai kwenu ni vema mkaweka na dirisha kwa ajili ya kuhamasisha wanaume kupima Virusi vya UKIMWI..Hivi karibuni Wazir Mkuu wetu Kassim Majaliwa amezindua kampeni ya kuhamasisha wananchi na hasa wanaume kupima Ukimwi. Hivyo niwaombe hata wanaume ambao wanakuja katika maoneshao nao wapime VVU.
“Niwapongeza NSSF kwa kazi nzuri ambayo mnaifanya nchini. Hata hivyo nitoe rai kwenu ni vema mkaweka na dirisha kwa ajili ya kuhamasisha wanaume kupima Virusi vya UKIMWI..Hivi karibuni Wazir Mkuu wetu Kassim Majaliwa amezindua kampeni ya kuhamasisha wananchi na hasa wanaume kupima Ukimwi. Hivyo niwaombe hata wanaume ambao wanakuja katika maoneshao nao wapime VVU.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mh. Jenista Mhagama akizungmza na Bw. Charles Lyimo mwanachama wa Shirika la Taifa la Hafadhi ya Jamii (NSSF) huku akiwa amembeba Mtoto Martin Lyimbo aliyemkuta katika banda la hilo wakati alipotembelea kwenye maonesho ya Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam na kukagua shughuli mbalimbali za (NSSF) leo. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mh. Jenista Mhagama akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa (NSSF) Godius Kahyarara wakati alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam leo, Kushoto ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Injinia Stella Manyanya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mh. Jenista Mhagama na Mkurugenzi Mkuu wa (NSSF) Godius Kahyarara wakimsikiliza Kaimu Meneja wa Uhusiano na Masoko Shirika la Hifadi ya Jamii (NSSF) Bw. Salim Khalfan wakati akitoa maelezo kwa waziri.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mh. Jenista Mhagama akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa (NSSF) Godius Kahyarara wakati alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam leo, Kushoto ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Injinia Stella Manyanya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mh. Jenista Mhagama na Mkurugenzi Mkuu wa (NSSF) Godius Kahyarara wakimsikiliza Kaimu Meneja wa Uhusiano na Masoko Shirika la Hifadi ya Jamii (NSSF) Bw. Salim Khalfan wakati akitoa maelezo kwa waziri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...