Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii.


 Waziri wa Habri, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amekubali kukaa na kujadiliana na Wadau wa utoaji huduma za Maudhui Mtandaoni kwa kina  na namna ya kulipia  tozo ua huduma hizo katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). 

 Akizungumza na watoa huduma hao mapema leo jijini Dar es Salaam, Dkt. Mwakyembe amesema kuwa Kanuni za Huduma hizo Mtandaoni zimetungwa na yeye Waziri mwenye dhamana ya Habari na TCRA ni Watekelezaji wa Sheria hizo.  ‘Milango bado ipo wazi kuhusu kanuni lakini zinarekebishika kukibainika kuwa na utata mkubwa, na pia kanuni hizi ni za wote’, amesema Dkt. Mwakyembe.

 Waziri huyo ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari na mtaalamu bingwa wa mambo sheria za mitandao, amesema kuwa kanuni hizo ni mpya ambapo wamekaa Wanasheria wa Wizara na Wataalam wa Mitandao kutoka TCRA kutengeneza kanuni hizo, hata hivyo amedai kila nchi inakuja kuiga mfano kwa Tanzania. 

 ‘Kanuni hizi zimetungwa kuangalia Mazingira ya nchi kutokana na Mitandao kuwa chanzo kikubwa cha Habari’, ameeleza Dkt. Mwakyembe Amesema Serikali ya Tanzania itafurahia kusimamia Kanuni ambazo zinaeleweka pamoja na kufuatwa na kila mtu.
 Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na michezo Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza mbele ya baadhi ya Waendesha mitandao ya kijamii mbalimbali (hawapo pichani), kuhusiana na changamoto wanazokumbana nazo kufuatia kuanza kwa utekelezaji wa kanuni za maudhui ya mtandaoni zilizoanza kutumika hivi karibuni,ambapo Waziri Mwakyembe amekubali kukutana na Wadau hao ili kuangalia maeneo ya kufanyiwa marekebisho kwa namna moja ama nyingine.

Mkutano huo umefanyika mapema leo katika ofisi za Radio7  Msasani  jijini Dar es Salaam ambapo waziri Mwakyembe alikuwa amealikwa.Pichani kulia ni Mwakilishi kutoka TCRA,Ndugu Kibaja sambamba na Mmiliki  na Mkurugenzi wa Radio 7  Online Antu Mandoza na kushoto ni Kaimu MKurugenzi Idara ya Habari MAELEZO,Patric Kipangula.
  Waziri wa Habri, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akitoa ufafanuzi kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo suala la kanuni za utoaji huduma za Maudhui Mtandaoni,alipokuwa akifanya mahojiano mafupi na kituo cha radio ya Mtandaoni Radio 7,Msasani Jijin Dar Es Salaam .  
 Mmoja wa Waendesha Mtandao wa DarMpya.Com John Marwa akiuliza moja ya swali kwa Waziri Mwakyembe kuhusiana  na kanuni/sheria za mtandao zilizoanza kutumika hivi karibuni,Mkutano huo umefanyika mapema leo katika ofisi za Radio7  Msasani  jijini Dar es Salaam ambapo waziri Mwakyembe alikuwa amealikwa.Pichani kulia ni Mwakilishi kutoka TCRA,Ndugu Kibaja sambamba na Mmiliki  na Mkurugenzi wa Radio 7  Online Antu Mandoza na kushoto ni Kaimu MKurugenzi Idara ya Habari MAELEZO,Patric Kipangulamapema leo 
 Sehemu ya Meza kuu ikichukua sehemu ya maoni yaliyokuwa yakitolewa na baadhi ya Wadau.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...