Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, akitoa ufafanuzi kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu namna Kituo cha Mafuta (KOJ) kinavyofanya kazi, wakati kamati hiyo ilipotembelea bandari ya Dar es Salaam.
Kaimu Meneja wa Kituo cha Mafuta (KOJ), Sixtus Karia akifafanua jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu namna meli zinavyopakua mafuta katika kituo cha hicho katika bandari ya Dar es Salaam, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa upanuzi wa bandari hiyo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Moshi Kakoso, akitoa maelekezo kwa uongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), wakati kamati hiyo ilipofanya ziara bandari ya Dar es Salaam.
Muonekano wa kazi zikiendelea kwenye mradi wa upanuzi wa gati namba 1 mpaka 7 katika bandari ya Dar es Salaam. Mradi huo unahusisha gati mpya ya kuhudumia meli za magari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...