Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (kushoto) baada ya kurejea kutoka jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam,walijadiliana  mambo mbalimbali yanayolihusu jeshi hilo. Akiwa mkoani Mbeya Mhe. Lugola amelivunja Baraza la Taifa la Usalama Barabarani na Kamati zote za Usalama barabarani za mikoa na wilaya zote, na kusema atayaunda upya ili kupambana na janga sugu la ajali za barabarani. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akipeana mikono na   Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye(kulia), baada ya kurejea kutoka jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Video courtesy of MCL Digital

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...