Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (kushoto) baada ya kurejea kutoka jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam,walijadiliana mambo mbalimbali yanayolihusu jeshi hilo. Akiwa mkoani Mbeya Mhe. Lugola amelivunja Baraza la Taifa la Usalama Barabarani na Kamati zote za Usalama barabarani za mikoa na wilaya zote, na kusema atayaunda upya ili kupambana na janga sugu la ajali za barabarani.
Video courtesy of MCL Digital
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...