Na Emanuel Madafa,Mbeya 

MAHAKAMA ya Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya imehairisha kutoa hukumu ya kesi ya jinai iliyokuwa ikimkabili Mbunge wa Chadema, Jimbo la Mbozi, Pascal Haonga na wenzake wawili.

Akihairisha kutoa hukumu hiyo leo, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Nemesi Chami, amesema hukumu hiyo imehairishwa mpaka  Agost, 10 mwaka huu, kutokana na majukumu mengi ya kimahakama pamoja na uzito wa kesi yenyewe. Upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili wa Serikali Joseph Pande akisaidiwa na Baraka Mgaya

Aidha, kesi hiyo ya jinai namba 117/2017 inawahusisha washitakiwa watatu ambao ni Mbunge Pascal Haonga, Mwenyekiti wa Kitongoji cha Karasha Mashaka Mwampashi na katibu wa Mbunge, Williferd Mwalusanya.

Imeelezwa kuwa Agosti 28 mwaka  2017, washitakiwa hao, wakiwa katika ukumbi wa ofisi za mamlaka ya Mji wa Mlowo, Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe, majira ya saa nane mchana, waliwazuia askari polisi kutekeleza majukumu yao, kufanya vurugu na kukataa kutoka nje ya ukumbi.

Washitakiwa wote watatu wapo nje kwa dhamana na kwamba wanatetewa na Wakili Boniphace Mwabukusi, ambaye aliunga mkono uamuzi wa mahakama hiyo kwa kuamini itatenda haki kwa pande zote mbili.

Baadhi ya wabunge wa Chadema, walijitokeza kusikiliza kesi hiyo akiwemo Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya Sophia Mwakagenda na Mbunge wa Jimbo la Tunduma, Franky Mwakajoka.
Mbunge wa Jimbo la Mbozi (Katikati ) akiwa na watuhumiwa wengine pamoja na wafuasi wa Chadema , katika kesi inayomkabili Mahakama ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...