Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimsikiliza Kaimu
meneja Uhusiano na Masoko wa Shirika la Hifadhi za Jamii (NSSF) Salim
Khalfan wakati akimpa maelezo alipotembelea kwenye banda la shirika hilo
katika maonesho ya Sabasaba yaliyomalizika na kufungwa leo kwenye
viwanja vya (TanTrade) Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam leo
katikati ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara ya Nje
(TanTrade) Bw. Edwin Rutageruka na kulia ni Afsa Uhusiano na masoko Bi
Angela Michael.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na baadhi
ya wafanyakazi wa (NSSF) mara baada ya kuwasili katika banda hilo leo
kwa lengo la kulitembelea.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Afisa
Uhusiano wa (NSSF) Bi Angela Michael wakati alipowasili katika banda
hilo.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akipokea zawadi kutoka
kwa Afisa Uhusiano na Masoko wa (NSSF) Bi. Angella Michael baada ya
kutembelea katika banda hilo.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika picha ya
pamoja na wafanyakazi wa (NSSF) mara baada ya kutembelea banda hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...