Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limedhamiria kutoa mafao yote sita yatolewayo ili kuisaidia sekta isiyo rasmi kujikinga na majanga mbalimbali na kujikwamua Kiuchumi

Akizungumza katika semina hiyo kwa viongozi wa vikundi vya ujasiriamali mkoani pwani, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng.Evaristi Ndikilo.

Alisema sekta isiyo rasmi ina kundi kubwa sana ambalo halijafikiwa na Hifadhi ya jamii hivyo ni fursa na muhimu kwa wale wote walio katika sekta hiyo wakiwemo mamalishe, bodaboda, wakulima, wavuvi, walio katika vikundi kama SACCOS na Vikoba kujiunga na NSSF ili waweze kujikinga na majanga mbalimbali.

Pia Mkuu wa mkoa ameongezea kuhimiza wajasiriamali wote wa Mkoa wa Pwani kujiunga na Mfuko wa hifadhi ya Jamii ili koungeza pato la Mkoa wa pwani na pia aliwahimiza viongozi mbalimbali wa serikali kuunga mkono mpango huu kwani utaisaidia serikali ya awamu ya tano katika mikakati ya kutatua changamoto mbalimbali zinazoikumba jamii.




Pia mkuu huyo wa mkoa amesema wajasiriamali wengi wanavilio vikubwa kwa kukosa mikopo na pia riba kubwa pindi warejeshapo mikopo hiyo..,Lakini amelipongeza sana shirika la Taifa la hifadhi ya jamii kuliona hilo na kukaa chini pamoja na Benki ya Azania kutoa mikopo kwa wajasiriamali wote na kwa riba nafuu kupitia vikundi vyao.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng. Evaristi Ndikilo akizungumza na Viongozi wa Vikundi vya uzalishaji mali wakati wa semina iliyoandaliwa na NSSF inayohusu Hifadhi ya Jamii kwa sekta isiyo rasmi.
Viongozi wa Vikundi vya uzalishaji mali wakiwa katika semina iliyoandaliwa na NSSF kwa ajili ya kuratibisha Hifadhi ya Jamii kwa sekta isiyo rasmi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...