*Ni katika ajali iliyoua watu watano, kujeruhi mmoja jana usiku

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Mbeya amethibitisha kufariki dunia kwa watu watano baada ya kutokea ajali ya kugongana  magari matatu jana usiku na kinachoendelea asubuhi ya leo ni kuiondoa miili ya watu wawili ambayo imeng'ang'ania katika gari.

Ajali hiyo imetokea jana usiku katika eneo la Mlima Igawilo nje kigogo ya Mji wa Mbeya Mjini na kusababisha video vya watu hao. 
Akizungumza na Michuzi Blog kwa njia ya simu asubuhi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya  Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,Urich Matei amesema katika ajali hiyo wote waliofariki ni wanaume na kwamba watu watatu walifanikiwa ukitoa miili yao eneo la ajali na kuipeleka chumba cha kuhifadhia maiti. 
"Kwa sasa asubuh hii tupo eneo ambao ajali imetokea kwani kuna miili ya watu wawili bado tunahangaika kuitoa katika gari. Imekandamizwa ndani ya gari ndogo aina ya Noah  ambayo ililaliwa na kontena. 

"Hivyo tunaendelea kuitoa miili ya watu hawa.Idadi ya watu waliokufa ni watano na majeruhi mtu mmoja. Chanzo cha ajali imetokana na lori ambalo limebeba kontena kufeli breki na kusababisha gea boksi kukatika na hivyo kupoteza muelekeo,"amesema Kamanda. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...