Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa ametembelea mradi mkubwa maji wa bwawa katika Mto Rufiji utakaoweza kusaidia matumizi ya maji kwenye kambi ya ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge)

Mradi huo unaotekelezwa Wizara ya Maji na Umwagiliaji kupitia  Mamlaka ya Maji safi na Maji taka (DAWASA) na umeweza kugharimu kiasi cha Milioni 604.9 ukiwa ni muendelezo wa mradi mkubwa wa maji unaoendelea Kisarawe.

Akizungumza baada ya kutembelea maporomoko ya Mto Rufiji Prof Mbarawa amesema kuwa mradi huo wa maji utakuwa na uwezo wa kuzalisha maji lita 209,000( laki mbili na elfu tisa) kwa ajili ya matumizi ya kambi ya ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).

Amesema, mradi huo wa maji utawasaidia wakandarasi kusa na miundo mbinu wezeshi itakayowapatia maji muda wote wa matumizi yao ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanusi mkubwa.

"Miundo mbinu wezeshi itawapa fursa wakandarasi wafabye kazi kwa ufanisi mkubwa sana kwa  sababu maji yatakuwa yanapatikana muda wote na kila siku na hili litasaidia katika kuhakikisha mradi wetu wa ujenzi wa bwawa la umeme kumalizika kwa muda ulipangwa,"amesema Prof Mbarawa.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akifunga bomba la kisasa la kusafirishia maji  kwenye eneo la kambi lenye jumla ya Km 1463,kipenyo cha nchi 1.5 na nchi 3 kwenye eneo la ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akifunikia bomba la kusafirishia majighafi kwenye eneo la kambi lenye jumla ya Km 1463,kipenyo cha nchi 1.5 na nchi 3 kwenye eneo la ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akiwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Dr Suphian Masasi wakiwa wanakagua  bwawa la kusafishia maji yanayotoka katika Mto Rufiji kwa ajili ya matumizi ya wakandarasi waujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makamd Mbarawa akirusha maji katika moja ya bwawa la kusafishia maji yanayotoka katika Mto Rufiji kwa ajili ya matumizi ya wakandarasi waujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge).
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa akiwa anakagua mradi mkubwa wa maji katika Bwawa la Mto Rufiji utakaoweza kuwasaidia wakandarasi kupata maji ya uhakika kwenye ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler's Gorge) akiambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Maji Taka (DAWASA) Dr Suphian Masasi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...