Na WAMJW CHATO - GEITA
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetangaza rasmi kuwa hakutakuwa na riba katika mikopo itakayotolewa kwa wanawake, vijana na walemavu katika ngazi ya Halmashauri.

Kauli hiyo imetolewa wilayani Chato na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokitembelea kikundi cha wanawake wajasiriamali cha Jikomboe.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuwasaidia Wanawake, vijana na walemavu kujikwamua kiuchumi hivyo imeona ni bora mikopo itolewe bila riba ili kuwapa fursa wanawake, vijana na walemavu kwa ajili ya kuanzisha miradi ya wingi ya kujikwamua kiuchumi.

Ameongeza kuwa suala la riba limekuwa kikwazo kwa makundi mengi kuweza kukopa na kurejesha mikopo kwa wakati.

"Niseme tu tumeliangalia suala hili kwa karibu ili tuwawezeshe wananchi hasa wanawake, vijana na walemavu kujikwamua kiuchumi" alisisitiza Dkt. Ndugulile.
 Mbunge wa Chato (CCM) na Waziri wa Madini Dkt. Medard Kalemani akimshukuru Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Faustine Ndugulile kwa ziara yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya Naibu Waziri huyo ya siku mbili mkoani humo.
 Mwekahazina wa kikundi cha Jikomboe kilichopo wilayani Chato Mkoani Geita akiwasilisha risala yao kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wkati wa kuhitimishwa kwa  ziara yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya Naibu Waziri huyo ya siku mbili mkoani humo.
 Baadhi ya wananawake wajasiriamali wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akihitimisha ziara  yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya siku mbili ya Naibu Waziri huyo mkoani humo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia malighafi inayotumika kutengeneza batiki wakati alipokitembelea kikundi cha wanawake wajasiriamali cha  Jikomboe kilichopo Wilaya ya Chato wakati akihitimishaziara  yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya siku mbiliua  Naibu Waziri huyo  mkoani humo.
Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...