Na WAMJW CHATO - GEITA
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetangaza rasmi kuwa hakutakuwa na riba katika mikopo itakayotolewa kwa wanawake, vijana na walemavu katika ngazi ya Halmashauri.
Kauli hiyo imetolewa wilayani Chato na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokitembelea kikundi cha wanawake wajasiriamali cha Jikomboe.
Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuwasaidia Wanawake, vijana na walemavu kujikwamua kiuchumi hivyo imeona ni bora mikopo itolewe bila riba ili kuwapa fursa wanawake, vijana na walemavu kwa ajili ya kuanzisha miradi ya wingi ya kujikwamua kiuchumi.
Ameongeza kuwa suala la riba limekuwa kikwazo kwa makundi mengi kuweza kukopa na kurejesha mikopo kwa wakati.
"Niseme tu tumeliangalia suala hili kwa karibu ili tuwawezeshe wananchi hasa wanawake, vijana na walemavu kujikwamua kiuchumi" alisisitiza Dkt. Ndugulile.
Mbunge
wa Chato (CCM) na Waziri wa Madini Dkt. Medard Kalemani akimshukuru
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile kwa ziara yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya
Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na
maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya Naibu Waziri huyo ya
siku mbili mkoani humo.
Mwekahazina
wa kikundi cha Jikomboe kilichopo wilayani Chato Mkoani Geita
akiwasilisha risala yao kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wkati wa kuhitimishwa
kwa ziara yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa
Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na maendeleo ya
jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya Naibu Waziri huyo ya siku mbili
mkoani humo.
Baadhi
ya wananawake wajasiriamali wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile
wakati akihitimisha ziara yake alioyoifanya katika kata za wilaya ya
Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji wa huduma za afya na
maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya siku mbili ya Naibu
Waziri huyo mkoani humo.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile akiangalia malighafi inayotumika kutengeneza batiki
wakati alipokitembelea kikundi cha wanawake wajasiriamali cha Jikomboe
kilichopo Wilaya ya Chato wakati akihitimishaziara yake alioyoifanya
katika kata za wilaya ya Chato mkoa wa Geita iliyolenga kuangalia utoaji
wa huduma za afya na maendeleo ya jamii wakati wa kuhitimisha ziara ya
siku mbiliua Naibu Waziri huyo mkoani humo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...