Na Zuena Msuya, Pwani,
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amesema Serikali kupitia Wizara ya Madini inaangalia namna bora ya kuimarisha soko la chumvi inayozalishwa nchini yenye uwezo wa kukidhi mahitaji ya ndani na ziada, kwa kuzuia ile inayoingizwa kutoka nchi za nje.
Nyongo alisema hayo, wilayani Bagamoyo mkoani Pwani, Julai 23, 2018, baada ya kutembelea Mgodi wa kuzalisha chumvi wa kampuni ya Stanley and Sons ulioanzishwa mwaka 1948/49 uliopo katika Kijiji cha Kitame wilayani humo.
Akizungumzia uzalishaji chumvi, Nyongo alitolea mfano mgodi pekee wa Stanley kuwa, huzalisha chumvi kati ya tani 4000 hadi 6000 kwa mwaka kulingana na hali ya hewa, licha ya kuwepo migodi mingi ya uzalishaji chumvi katika baadhi ya Mikoa nchini ambapo mara nyingi wazalishaji wamekuwa wakilalamikia ukosefu wa soko la chumvi wanayozalisha.
Alitaja baadhi ya Mikoa iliyokuwa na migodi ya kuchimba na kuzalisha chumvi kuwa ni pamoja Pwani yenye zaidi ya mgozi mmoja, Kigoma katika eneo la Uvinza, Lindi pamoja na Mtwara.
" Tanzania ina migodi mingi ya kuchimba na kuzalisha chumvi bora, ya kutosha na yenye kukidhi mahitaji ya ndani na kuuza nje, hivyo ni wakati sasa, serikali kuangalia namna bora ya kulinda soko la ndani la chumvi kwa kuzuia ile inayoingizwa kutoka nje, ili wazalishaji waweze kupata soko la uhakika", alisisitiza Nyongo.
Aidha aliwaagiza wachimbaji na wazalishaji wa chumvi nchi, kusindika chumvi hiyo katika ubora unaotakiwa na kukidhi viwango vya soko la Kimataifa kwa kuzingatia kuwa, Tanzania inazalisha chumvi iliyobora.
Sambamba na hilo, alieleza kuwa kwakuwa chumvi ni bidhaa mtambuka inayotumika kama chakula, dawa, pamoja na kuwa ni madini hivyo, aliwataka wachimbaji na wazalishaji wa chumvi, kusindika chumvi hiyo katika ujazo tofauti na kwa bei nafuu ili kila mmoja aweze kumudu gharama za kununua chumvi hiyo kwa matumizi husika ikiwemo majumbani, viwandani na hata katika mifugo.
Naibu Waziri  Stanslaus Nyongo( aliyeinama) akigusa chumvi iliyorundikwa tayari kwa kufungashwa katika mifuko kwa ajili ya kuuzwa kwa watumiaji.
 Baadhi ya vitalu vya kuzalisha chumvi katika mgodi wa kampuni ya Stanley and Son, uliopo katika Kijiji cha Kitame wilayani Bagamoyo mkoani Pwani. 
Naibu Waziri,  Stanslaus Nyongo,(kulia) akiingia katika moja ya vitalu vya mgodi wa chumvi wa kampuni ya Stanley and Sons.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...