Profesa James K. Shaba anasikitika kutangaza kifo cha mke wake, Elizabeth E. Shaba, kilichotokea Chicago IL, Marekani. 
Marehemu, aliyekuwa na miaka 80 aliaga dunia Jumapili, tarehe 1 Julai, 2018 nyumbani kwake akiwa amezungukwa na watoto na wote waliompenda. 
 Marehemu alizaliwa Disemba 21, mwaka 1937 kijijini Mbokomu Moshi, Tanzania. Alikuwa ni mtoto wa tano kati ya watoto nane wa familia ya mzee Elisa Kileo Mrema na Anale Mhache Mrema. Habari hizi ziwafikie ndugu, jamaa na rafiki wote mahali popote walipo. 
Mazishi ya marehemu yatafanyika siku ya Jumamosi tarehe 7 Julai, 2018.

Anuani: Montclair-Lucania Funeral Home, 
6901 W. Belmont Ave 
Chicago IL, 60634
Muda ni saa 9 jioni, na kufuatiwa na sala saa 11 jioni. Wote mnakaribishwa.
Bwana alitoa, na Bwana ametwaa.
Jina la Bwana na lihimidiww
AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...