Na Dotto Mwaibale

WATUMIAJI wa mitandao wametakiwa kujua haki na wajibu wanapotumia mtandao ili kuondoa mikanganyiko inayoweza kujitokeza kwa watumiaji dhidi ya serikali na makundi mengine.

Hayo yalisemwa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na Mratibu wa Jukwaa la Utawala wa Mtandao (TzIGF), Rebecca Ryakitimbo wakati wa kufunga kongamano la kujadili matumizi ya mtandao na utawala.

Alisema ni vizuri watumiaji wa mtandao wakajua haki na wajibu wakati wa matumizi ya mtandao.Ryakitimo alisema hapa nchini limeundwa jukwaa la utawala wa mtandao litakaloshughulikia kutoa elimu juu ya masuala ya mtandao ikijumuisha masuala ya kisheria, wajibu wa mtumiaji wa mtandao pamoja na kutoa mapendekezo ya watumiaji wa serikalini katika kutengeneza sera zenye tija kwa mamlaka na watumiaji.

Alisema matumizi ya mtandao yamekuwa ni sehemu ya maisha ya binaadamu wa sasa ya kila siku ambapo watu wamekuwa wakitumia kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kujiajiri, kuwasiliana na hata kutoa na kupata elimu pia, kadri mawasiliano hayo ya mitandao yanavyozidi kukua, ndivyo mamlaka nazo zimeweza kuunda sera na sheria kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia ya mitandao. 

Aliongeza kuwa Umoja wa Mataifa nao uliunda jukwaa linaloshughulikia haki na wajibu wa watumiaji wa masuala ya mtandao, UNIGF. Hivyo hata nchi wananchama nao wameunda majukwaa kama hayo ili kuwa na kauli moja katika kutunga sera zinazokubalika kwa mamlaka na watumiaji ili kuleta usawa unaoleta uwajibikaji katika mitandao. 
Mwanasheria kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) Dkt. Philip Filikunjombe, akizungumza wakati wa kufunga kongamano la kujadili matumizi ya mtandao na utawala lililofanyika Chuo cha Usafirishaji (NIT) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 
Washiriki wakiwa kwenye kongamano hilo.
Washiriki wakiwa kwenye kongamano hilo.
Mratibu wa Jukwaa la Utawala wa Mtandao (TzIGF), Rebecca Ryakitimbo, akizungumza katika kongamano hilo kuhusu matumizi ya mtandao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...