Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
KAMPUNI ya Simu za Mkononi ya Vodacom imepata leseni ya masafa ya mawasiliano katika bendi ya 700MHZ baada ya kuibuka mshindi katika mnada wa masafa hayo.
Vodacom ilishinda masafa hayo kwa jumla ya bei dola za Kimarekani 1,0005,000 ambapo masafa hayo yatalipiwa kodi kila mwaka dola za Kimarekani 40,000.
Akizungumza baada ya Vodacom kupata leseni Waziri wa Ujenzi , Mawasiliano na Uchukuzu Mhandisi Isaac Kamwelwe amesema kuwa TCRA imekuwa ikifanya kazi nzuri ambapo imetoa gawio la sh.bilioni 81.Amesema kuwa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) kuhakikisha Vodacom inatekeleza masharti ya leseni yanatekelezwa kama ilivyokusudiwa katika utoaji wa huduma ya mawasiliano.
Kamwelwe ameiataka TCRA kuendelea na utaratibu wa kugawa masafa kwa njia ya mnada kutokana na faida ya kiuchumi kwa fedha inayopatikana kuendeleza miundombinu ya huduma za simu za mikononi na data zenye kasi kubwa , ubora , kupunguza gharama za uwekezaji.Nae Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhadisi James Kilaba amesema kuwa kuna njia mbalimbali za ugawaji wa masafa ikiwemo kutoa masafa kwa anayewahi kuomba pamoja na njia ya mnada.
Amesema masafa ya simu za mkononi ya faida katika kuendeleza huduma za simu za mkononi na data zenye ubora ,kupunguza gharama za matumizi ya huduma za mawasiliano kwa mtoa huduma ya masafa hayo.Kilaba amesema faida nyingine ni kukuza na kuchochea ubunifu wa huduma mpya na matumizi ya teknolojia za habari na mawasiliano pamoja na serikali kupata mapato kutokana na mauzo ya masafa hayo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
Mhandisi James Kilaba akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom
Tanzania Plc Hisham Hendi, leseni ya Masafa ya 700MHz, iliyotolewa
na Mamlaka hiyo kwa kampuni ya Vodacom baada ya kuibuka mshindi katika
mnada ulioendeshwa na TCRA mwezi Juni mwaka huu. Hafla hiyo imefanyika
jijiji Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo
cha Sheria wa Vodacom Tanzania Plc, Olaf Momburi na Mkuu wa Kitengo cha
Udhibiti (Head of Regulatory Affairs) wa Kampuni hiyo Ngayama Matongo.
Waziri
wa ujenzi ,Uchukuzi, na Mawasiliano, Mhandisi Isaac Kamwelwe
akiupongeza uongozi wa Vodacom wakati wa hafla ya kukabidhiwa leseni
ya masafa ya 700MHz, iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA), Vodacom ilibuka mshindi wa mnada wa masafa ya Mawasiliano
uliofanywa na TCRA. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom
Tanzania, Hisham Hendi, Kaimu Mkurugenzi wa kitengo cha Sheria Olaf
Momburi na Mkuu wa kitengo cha Udhibiti (Head of Regulatory Affairs) wa
Vodacom Tanzania Plc Ngayama Matongo.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini TCRA, Mhadisi James Kilaba
akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na utoaji wa leseni ya
masafa kwa kampuni Vodacom katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa TCRA
jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Hisham Hendi, akiongea wakati
wa hafla ya kukabidhiwa leseni ya masafa ya 700MHz, iliyotolewa na
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kampuni hiyo baada ya kuibuka
mshindi katika Mnada uliondeshwa na TCRA mwezi Juni mwaka huu. Hafla
hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi, Mambo ya Watumiaji na Viwanda (DCIA) wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Raynold Mfungahema (kushoto) akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Plc, Hisham Hendi wakati wa hafla ya kukabidhiwa leseni ya Masafa ya Mawasiliano katika bendi ya 700MHz iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) baada ya Vodacom kuibuka mshindi katika mnada ulioendeshwa na TCRA. Hafla hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania Plc wakiwa kwenye hafla ya kampuni hiyo kukabidhiwa leseni ya Masafa ya Mawasiliano katika bendi ya 700MHz iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) baada ya Vodacom kuibuka mshindi katika mnada ulioendeshwa na TCRA. Hafla hiyo imefanyika Makao makuu ya TCRA jijini Dar es Salaam.
Waziri wa ujenzi, Uchukuzi, na Mawasiliano, Mhandisi Isaac Kamwelwe (kushoto)akimpongeza kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Plc, Hisham Hendi wakati wa hafla ya kukabidhiwa Leseni ya Masafa ya 700MHz, na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) iliyofanyika makao makuu ya Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam, Vodacom ilibuka mshindi wa mnada wa masafa ya Mawasiliano uliofanywa na TCRA.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...