Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii

Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) imefanikisha kuboresha uzalishaji wa maji katika mtambo wa Mtoni baada ya kununua na kufunga pampu mpya za kusukuma majighafi kutoka katika mto Kizinga.

Uzalishaji huo umeongezeka baada ya jumla ya pampu mbili zenye uwezo wa kusukuma maji kwa kiasi cha mita za ujazo 140 kwa saa kwa kila pampu moja ambazo zinafanya kazi kwa ufanisi.

Taarifa hiyo imetolewa jana jioni na ofisi ya uhusiano wa jamii DAWASA baada ya kumalizika kufungwa kwa mtambo huo uliogarimu jumla ya sh. Milioni 239.1

" kufungwa kwa pampu hizo kumeongeza uwezo wa kusukuma maji na hivyo kurejesha uwezo wa mtambo wa Mtoni kuzalisha maji kwa ajili ya wakazi na waty wenye viwanda katika eneo hilo la Temeke wanaopata maji kutoka katika mtambo huo". Imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Ameongeza kuwa, Mtambo wa Mtoni uliojengwa mwaka 1974, ndio mkongwe kuliko yote inayozalisha maji katika eneo la Huduma la DAWASA ukiwa unazalisha lita milioni tisa za maji kwa siku.
Aidha Msuya amevitaja vyanzo vingine vya maji vilivyopo DAWASA ni, Ruvu Juu, Ruvu Chini, na Visima Virefu vilivyopo katika maeneo mbali mbali jijini ambayo yanaweza kusaidia mahitaji ya maji jijini Dar, ambayo yanafikia Lita milioni 544 kwa siku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...