Na Frankius Cleophace Tarime.

Waliokuwa Ngariba Wilayani Tarime Mkoani Mara wamepatiwa Mafunzo ya Ujasiriamali kwa lengo la kujikwamua Kiuchumi ili wasirudie tena suala Ukeketaji kwa Mtoto wa ni baada ya kupatiwa Elimu juu ya Madhara ya Ukeketaji kwa Mtoto wa Kike.

Ngariba hao wamedai kuwa kipindi cha Ukeketaji hupata pesa Nyingi zinazotokana na Ukeketaji jambo ambalo uwangumu kuacha kitendo hicho licha ya Mashirika mbalimbali likiwemo Shirika la AFGM Masanga kuendelea kutoa Elimu juu ya Madhara ya Ukeketaji ili Jmii iweze kubadilika.

Kwa kuliona hilo Shirika la ATFGM Masanga ambao ni wadau wa Kupinga Ukatili katika Jamii wameamua kutoa Mafunzo ya Ujasiriamali kwa Waliokuwa Ngariba lakini kwa sasa wameachana na Kitendo hicho baada ya kupewa Elimu ili waweze kufanya kazi zinazotambulika na Serikali kwa lengo la kujipatia kipato na siyo kutegemea tena Ukeketaji.

Mafunzo hayo ya Ujasirimali pia yamewashirikisha Mabinti lengo ni kuwajengea Uwezo ili kuendelea kutoa Elimu hiyo katika Jamii inayowazunguka huku walikuwa Ngariba hao wakipatiwa Mafunzo ili kuendeleza Biashara zao na kuondokana na mawazo ya kurudia kukeketa tena.

Wamedai kuwa katika Kukeketaji wamekuwa wakipata zaidi ya Mill Nane mpaka Tisa Ukeketaji unamalizika huku Binti Mmoja akikeketwa kuanzia Elfu Kumi na zaidi.“Sisi kipindi cha Ukeketaji tulikuwa tunapata Pesa Nyingi lakini kwa sasa wazee wamekataa hatutakeketa tena hivyo tunaomba Serikali itupatie Mitaji baada ya Mafunzo haya tuliyoyapata” alisema Mmoja wa Walikuwa Ngariba.

Mgeni rasmi ambaye ni Katibu wa Afya Wilaya ya Tarime Neema Alphonce akikabidhi cheti cha Mafunzo ya Ujasiriamali kwa mmoja wa waliokuwa ngariiba baadaya kupata Elimu hiyo.
Picha ya pamoja na Mgeni rasmi na Washiriki baada ya kupata Mafunzo 
Mkurugenzi wa Shirika la ATFGM Masanga Sister Stella Mgaya akiongea na Washiriki wa Mafunzo hayo na kusisitiza suala kuendelea kuelimisha jamii katika Maeeo wanayotoka.
Washiriki wakiendelea na Mafunzo hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...