Kamati ya bunge ya kudumu inayosimamia miundo mbinu,Mwenyekiti wa kamati Ndugu Seleman Kakoso,wakiambata na Katibu  Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Uchukuzi Dkt.Leornad Chamuriho pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania, Ndugu Masanja Kadogosa,kukagua njia ya reli Tanga,Moshi,Arusha kwa lengo la kufanya maandalizi ya Uboreshaji wa njia ili iweze kafanya kazi kama awali.


Shirika la Reli linaendelea na mikakati ya  ufufuaji wa njia za reli zilizokuwa hazifanyi kazi kwa muda mrefu na kuboresha reli zinazoendelea kutoa huduma bora za uhakika kwa gharama nafuu, kukamilika kwa mikakati kunatarajia kuongeza tija katika kuendeleza na kukuza uchukuzi wa viwanda Nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Ndugu Masanja Kadogosa akitoa maelezo kwa kamati ya bunge ya kudumu inayosimamia miundo mbinu mikakati ya Uboreshaji wa njia ya Reli Tanga,Arusha ,Moshi baada ya kusimama kutoa huduma kwa takribani miaka kumi. 
Kamati ya bunge ya kudumu inayosimamia miundo mbinu ikiendelea kupata ufafanuzi wa Uboreshaji wa njia ya Reli Tanga,Arusha na Moshi walipofanya ziara ya kutembelea njia hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...