Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Bi. Mindi Kasiga Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, alipotembelea banda la Wizara.
Mhe. Mahiga akisikiliza maelezo kutoka kwa watumishi wa Wizara kwenye maonesho ya biashara ya kimataifa
Mhe. Mahiga akiwa kwenye banda la kituo cha kumbi za mikutano cha kimataifa (AICC) kwenye maonesho ya biashara ya sabasaba. Mbele yake ni baadhi ya watumishi wa kituo hicho.
Mhe. Mahiga akikabidhiwa zawadi ya mchoro na Bibi Hoyce Temu kutoka Kitengo cha Mawasiliano cha Umoja wa Mataifa (UN). Waziri Mahiga alitembelea banda la UN kwenye maonesho ya sabasaba na kupata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...