Na Agnes Francis, globu ya jamii.
Hatimaye klabu ya mbaofc wamefanikiwa kuinasa saini ya mchezaji Zam Elias Zamfuko aliyekuwa akichezea timu ya Afrikan Lyon.
Katika makubaliano baina yao kiungo mkabaji huyo ataitumikia klabu hiyo yenye makao makuu kanda ya ziwa mkoani mwanza kwa misimu miwili.
Klabu hiyo iliyomaliza msimu wake kwa kusua sua kwa sasa imefikisha jumla ya wachezaji 3 katika muendelezo wa usajili wake.
Ni katika harakati za kujiandaa na msimu ujao wa vodacom Tanzania bara (VPL) 2018-2019 inayotarajia kuanza hivi karibuni.
Kiungo mkabaji zam Elias Zamfuko alietokea african lyon akiwa ameshikilia jezi ya waajiri wake wapya mbao fc baada ya kusaini mkataba miwili katika klabu hiyo.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...