Na Agnes Francis, globu ya jamii.

Hatimaye klabu ya mbaofc wamefanikiwa kuinasa saini ya mchezaji  Zam Elias Zamfuko aliyekuwa akichezea timu ya Afrikan  Lyon.

Katika makubaliano baina yao kiungo mkabaji  huyo ataitumikia klabu hiyo yenye makao makuu kanda ya ziwa  mkoani mwanza kwa misimu miwili.

Klabu hiyo iliyomaliza msimu wake kwa kusua sua kwa sasa imefikisha jumla ya wachezaji 3 katika muendelezo wa usajili wake.

Ni katika harakati za kujiandaa na msimu ujao wa vodacom Tanzania bara  (VPL) 2018-2019 inayotarajia  kuanza hivi karibuni.
Kiungo mkabaji zam Elias Zamfuko alietokea african lyon akiwa ameshikilia jezi ya waajiri wake wapya  mbao fc baada ya kusaini  mkataba miwili  katika klabu hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...