Na Karama Kenyunko,Globu ya jamii

WATU wawili wamefariki dunia na wengine 10 kujeruhiwa baada ya Basi la Modern Coach lililokuwa likitokea nchini Kenya kuja Dar es salaam kupata ajali katika eneo la Mbwewe, mkoani  Pwani.

Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Bw. Aminiel Aligaeshi amethibitisha kupokea majeruhi hao leo  saa 12 asubuhi.  
Akizungumza na Michuzi Blog Aligaeshi amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti na majeruhi wote 10 ambao wamewapokea wanaendelea vizuri. Kwa mujibu wa taarifa ni kwamba gari iliyopata ajali jali basi hilo lilikuwa na abiria 45, dereva mmoja na tingo mmoja na abiria 43.
Wakati huo huo basi la Maning nice lililokuwa likitokea Dar kwenda Masasi limepata ajali baada ya kugonga basi la Tashrif kwa nyuma na kisha kugonga magari mawili aina ya Coaster.
Ajali hiyo imetokea baada ya basi  hilo la Maning nice kuovatake eneo baya na kushindwa kurudi sehemu yake. Shuhuda wa ajali hiyo ameeleza kuwa katika Coaster hiyo, watu wengi wameumia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...