*Atumia saa milioni 2.4 ya kazi bila kupata ajali.
*Mwakilishi JICA ataja vipaumbele miradi ya maendeleo
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
MWAKILISHI Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan(JICA) nchini Tanzania Toshio Nagase amesema Mkandarasi wa kijapani amefanikiwa kuweka rekodi ya usalama wakati wa ujenzi Fly over ya Tazara ambapo kwa zaidi ya saa milioni 2.4 ya kazi yamepita bila ajali.
Amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anaelezea namna JICA wamekuwa wakishiriki katika kutoa misaada ya mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya miradi ya kimaendeleo.
Amefafanua JICA imekuwa inatekeleza miradi mbalimbali hapa nchini tangu mwaka 1963 na kwamba Watanzania 18,000 wamepata mafunzo Japan, wataalam 2,000 wa Japan wamekuja nchini.Pia watalaam wa kujitolea kutoka nchi hiyo 1600 wameletwa Tanzania kwa nyakati tofauti.
Hivyo wakati anazungumzia ujenzi wa Fly over hiyo amesema mkandarasi Japan ameweka rekodi kwani hadi sasa hakuna aliyepata ajali.
“Barabara ya juu ya kwanza yenye urefu wa mita 425 ambayo itakamilika Septemba mwaka huu.Msongamano wa magari kwenye makutano ya barabara yenye magari mengi hapa nchini utapungua kwa kiasi kikubwa.
Mwakilishi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan(JICA) Ofisi ya Tanzania Toshio Nagase akizungumza leo jijini Dar es Salaam ya miradi mbalimbali ya maendeleo.

Jinsi barabara ya flyover ilivyo.
Baadhi ya wajumbe kutoka JICA wakifurahia kukamilika kwa ujenzi wa Fly over ya Tazara jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...