Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii.

RUBANI wa kampuni ya ndege ya Tanzania, (ATCL), Sadiki Jabez, ameieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, ATCL ililipia garama za matengenezo ya ndege iliyokodishwa licha ya kwamba matengenezo hayo yalifanywa na kampuni iliyowakodisha.
 Jabez ambaye pia ni mkurugenzi muendeshaji wa ATCL na  shahidi wa tisa wa upande mashtaka ameeleza hayo leo Agosti 29 wakati akitoa ushahidi wake dhidi ya kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh. Bilioni 71, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Augustino Rwenzile.
Mattaka anadaiwa kusababisha hasara hiyo kutokana na kusaini mkataba wa kukodi ndege bila kufuata Sheria ya manunuzi ya umma pamoja na ushauri wa kiufundi.
Akiongozwa na wakili wa Serikali, Timon Vitalis, amedai, mwenye jukumu la kutengeneza ndege pale inapokuwa inahitaji marekebisho  hujulikana kutokana na jinsi mkataba ulivyoingiwa lakini hakuwahi kuuuona huo mkataba.
Shahidi Jabez amedai mwaka 2007, ATCL ikiwa chini ya mkurugenzi David Mataka ilikuwa na ndege moja, 737 boing.
 Amedai, baadae ATCL waliazimia kukodisha ndege airbus 320 kutoka kampuni ya Wallis.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...