Na Mwandishi Wetu
BONDIA Vicent Mbilinyi amesaini mkataba wa kuzipiga na Saidi Mpoma ‘Kidedea’ septemba 15 katika uwanja wa ndani wa Taifa
akizungumza mara baada ya kusaini mkataba uho mbilinyi amesema kuwa atafanya mazoezi ya kutosha ili aweze kushinda kwa kuwa ngumi kwake ni kazi kazi na kuwataka mashabiki wake wote kujitokeza siku hiyo kushudia mpambano uho kwani ato waangusha amejipanga vizuri
Nae Saidi Kidedea amesema anashukuru kwa kupata mpambano uho kwana yeye siku zote achaguwi mabondia kwake yoyote anaekuja mbele yake kazi anayo na amepanga kummaliza mpinzani wake katika raundi za awali ili asiwachoshe mashabiki anao wategemea
aidha ameomba wapenzi wa mchezo wa masumbwi waje kumsapoti kwani ato wahangusha ata kidogo
Na mratibu wa mpambano huo Rajabu Mhamila ‘Super D’ amesema siku hiyo kutakuwa na mapambano makubwa ambapo bondia Fred Sayuni atapambana na Haidari Mchango wakati George Dimoso atavaana na Abdallah Pazi ‘Dulla Mbabe’ na Imani Mapambano ataoneshana umwamba na Paul KamataSadiki Momba atavaana na Mohamed Kashinde na bondia machachari Tonny Rashidi atavaana na Said Zungu Ramadhani Shauri atakumbana na Saidi Amani
Mbali na mipambano hiyo ya ngumi siku hiyo pia kutakuwa na burudani mbali mbali za muziki
Mabondia Saidi Mpoma ‘Kidedea’ kushoto akitunishiana misuli na Vicent Mbilinyi baada ya kusaini mkataba wa kuzichapa Septemba 15 katika uwanja wa ndani wa Taifa Picha na SUPER D BOXING NEWS.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...