Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
MTENDAJI Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) Profesa Dos Santos Silayo ameelezea jitihada mbalimbali zinazofanyika nchini katika kulinda na kuhifadhi uoto wa misitu asili nchini.
Amesema hayo akiwa eneo la Msitu wa Kazimzumbwi wilayani Kisarawe mkoani Pwani wakati wa uzinduzi wa jitihada za Tanzania kuungana na nchi nyingine za Afrika katika kuhifadhi na kuendeleza hifadhi za misitu
Mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo alikuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Japhet Hasunga pamoja na mwenyeji wao Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo ambaye alitumia nafasi hiyo kuelezea jitihada zinazofanyika kulinda misitu iliyopo wilayani kwake.
Akizungumza kwenye tukio hilo Profesa Silayo amefafanua Tanzania ni mwanachama wa Afrika katika juhudi hizo za kuhifadhi na kuendeleza hifadhi za Misitu African Forest Landscape Restoration Initiatives (AFR100).
Amesema lengo kuu la juhudi hizo ni kurejesha Uoto wa Asili kwa bara la Africa kwa hekta millioni 100 ifikapo mwaka 2030 na kwamba mkakati huo ulijadiliwa na kukubalika katika mkutano wa 14 wa Misitu uliofanyika nchini Afrika Kusini mwaka 2015.
Ambapo uliliona suala hili na kuanzisha mkakati huu wa Nchi za Afrika. Pia mkatati huo wa Afrika ni kwa ajili ya kuchangia mkatati wa Dunia (Bonn Challenge) wenye lengo la kurejesha uoto wa asili kwa hekta milioni 150 ifikapo mwaka 2020 na hekta milioni 350 ifikapo mwaka 2030.
MTENDAJI Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) Profesa Dos Santos Silayo ameelezea jitihada mbalimbali zinazofanyika nchini katika kulinda na kuhifadhi uoto wa misitu asili nchini.
Amesema hayo akiwa eneo la Msitu wa Kazimzumbwi wilayani Kisarawe mkoani Pwani wakati wa uzinduzi wa jitihada za Tanzania kuungana na nchi nyingine za Afrika katika kuhifadhi na kuendeleza hifadhi za misitu
Mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo alikuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Japhet Hasunga pamoja na mwenyeji wao Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo ambaye alitumia nafasi hiyo kuelezea jitihada zinazofanyika kulinda misitu iliyopo wilayani kwake.
Akizungumza kwenye tukio hilo Profesa Silayo amefafanua Tanzania ni mwanachama wa Afrika katika juhudi hizo za kuhifadhi na kuendeleza hifadhi za Misitu African Forest Landscape Restoration Initiatives (AFR100).
Amesema lengo kuu la juhudi hizo ni kurejesha Uoto wa Asili kwa bara la Africa kwa hekta millioni 100 ifikapo mwaka 2030 na kwamba mkakati huo ulijadiliwa na kukubalika katika mkutano wa 14 wa Misitu uliofanyika nchini Afrika Kusini mwaka 2015.
Ambapo uliliona suala hili na kuanzisha mkakati huu wa Nchi za Afrika. Pia mkatati huo wa Afrika ni kwa ajili ya kuchangia mkatati wa Dunia (Bonn Challenge) wenye lengo la kurejesha uoto wa asili kwa hekta milioni 150 ifikapo mwaka 2020 na hekta milioni 350 ifikapo mwaka 2030.

Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Profesa Does Santos
Silayo(kulia) pamoja na Mkurugenzi mkazi wa WWF Tanzania Dk.Amani
Ngusaru(kushoto) wakisaini mkataba wenye
lengo la kulinda na kuhifadhi msitu wa Kazimzumbwi ,Ruvu Kusini na
Vikindu wilayani Kisarawe.Wanaoahuhudia ni Mkuu wa Wilaya Kisarawe
Jokate Mwegelo na Naibu Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii Japhet
Hasunga.

Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Profesa Does Santos
Silayo(kulia) akiwa ameshikana mkono na Mkurugenzi mkazi wa WWF Tanzania
Dk.Amani Ngusaru baada ya kusaini mkataba wenye lengo la kulinda na
kuhifadhi msitu wa Kazimzumbwi ,Ruvu Kusini na Vikindu wilayani
Kisarawe.Wanaoahuhudia ni Mkuu wa Wilaya Kisarawe Jokate Mwegelo na
Naibu Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii Japhet Hasunga.

Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Profesa Does Santos
Silayo(kulia) pamoja na Mkurugenzi mkazi wa WWF Tanzania Dk.Amani
Ngusaru wakiwa wameshika mikataba mara baada ya kusaini mkataba wenye
lengo la kulinda na kuhifadhi msitu wa Kazimzumbwi ,Ruvu Kusini na
Vikindu wilayani Kisarawe.Wanaoahuhudia ni Mkuu wa Wilaya Kisarawe
Jokate Mwegelo na Naibu Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii Japhet
Hasunga.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...